Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

SERIKALI imesema kuwa itapitia mikataba yote katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere pamoja na kufanya mabadiliko ya uongozi huo kutokana na kufanya kazi kwa mazoea.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa wakati alipotembelea uwanja wa ndege huo baada ya kuwepo kwa taarifa ya wasafiri wakichukua muda mrefu kutoka uwanjani hapo.

Mbarawa amesema kuwa watu wanapoingia kutoka nje ya nchi wanaanza kusoma Tanzania ilivyo ikiwemo na uwanja wan degu kukaa kwa muda mrefu kutokana na mifumo ya watu kushindwa kujipanga.

Amesema kuwa mikataba katika uwanja huo wameingia wale watu waliofanya mikataba hawakuangalia masilahi ya nchi ndio maana mapato yanakuwa kidogo tofauti na ilivyo katika uhalisia.

Aidha amesema kuwa watakaa kikao kimoja kati ya watoa huduma katika uwanja wa mwalimu Julius Nyerere wakiwemo Idara ya Uhamiaji pamoja na benki ambako ndio inafanya watu wakae muda mrefu.

Nae Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Salim Msangi amesema kuwa wanazifanyia kazi changamoto ambazo Wazari amezianisha licha ya kuwa na miundombinu finyu.

Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuangalia utoaji huduma katika uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Salim Msangi akizungumza na waandishi wa habari juu Uboreshaji wa Huduma katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere leo.
Waziri Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akipata maelezo KaimuMkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Josepp Nyahende alipofanya ziara katika uwanja huo leo .
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akipata maelezo Afisa Maidizi wa Ushuru uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Hezron Gibe jinsi wanafanya kazi katika uwanja huo.
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akipewa maelezo na watoa huduma Ushuru uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere leo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...