Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo amesema apendezi kabisa kuona shughuli za
Ujenzi wa Majengo mapya zinaadhiri majengo ya kale bila sababu za msingi au
kuridhiwa na Serikali.
Akitoa
salama za Umoja wa nchi za Ulaya Balozi
wa Umoja wa Nchi za Ulaya hapa nchini Mh Roeland Van De Geer wanesema Umoja huo
unajisikia furaha kushiriki katika uhifadhi wa uridhi wa histori ya Tanzania
hasa kwa kupitia majengo ya kale na kuahidi kuendelea kuunga mkono jitihada
zinazofanywa na serikali katika uhifadhi huo.
Nae
Rais wa Wasanifu majengo nchini Mwandisi Henry. L.M. Mwoleka amewashau wananchi
na taarisis mbali mbali kuacha kabisa kubomoa majengo ya kihistoria nchini ili
kuendelea kuhifadhi majengo haya kama alama ya historia ya nchi yetu.
Akitoa
salama za shukrani Mea wa Jiji la Dar es Saalam Mh Isaya Mwita ameushukuru
Umoja wa Nchi za Ulaya na wadau mbali mbali kwa kufadhili ukarabati wa jengo
hilo la Kale na kuendelea kutoa wito kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam
kushiriki kikamilifu katika utunzaji wa Utamaduni huu wa Kihistoria kwani
kwakufanya hivyo jiji la Dar es Salaam litaingiza mapato mengi kupitia Utalii.
Naibu katibu Mkuu wa wizara hiyo Mh Nuru
Milano (kulia) na Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya hapa nchini Mh Roeland Van De Geer
wakifungua rasmi jengo la Kihistoria la Old Boma lililopo jiji Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa kituo cha Uridti wa
Ubunifu Majengo Bi Aida Mulokozi akitoa
malezo ya onesho maalum lililopondani ya jengo la OLD BOMA, pembeni yake ni
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mh Isaya Mwita na wageni wengine
wakimsikiliza kwa makini.
Wageni mbali mbali
walioudhuria sherehe hizo za ufunguzi wakiangalia onesho maalum lililopondani
ya jengo la OLD BOMA
Muonekano wa Jengo la kale la OLD BOMA
lililopo eneo la Posta jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...