Serikali imerudisha utaratibu wa kugawa vyandarua vyenye viuatilifu kwa akina mama wajawazito na watoto ambao wanapatiwa chanjo ya surua kupitia vituo vya kutolea huduma za afya ya uzazi na mtoto ambapo utaratibu huo utaanza rasmi mwezi Agosti mwaka huu.

Afisa Muuguzi kutoka Wizara ya Afya Epifania Malingumu amewaambia wajumbe wa mkutano wa uelimishaji juu ya mpango endelevu wa ugawaji vyandarau vyenye viuatilifu vya mda mrefu kuwa kwa sasa vyandarua hivyo havitapatikana katika maduka kama ilivyokuwa kwenye utaratibu wa ‘hati punguzo’ ya zamani.

Malingumu amesema hapo awali vyandarua vyenye viuatilifu vilikuwa vikitolewa kwa mfumo wa hati punguzo ambapo mama mjamzito alikuwa anatakiwa kutafuta maduka ya mawakala wa vyandarua hivyo mara baada ya kupatiwa hati hiyo katika vituo vya kutolea huduma ya afya ya uzazi.

“Utaratibu wa hati punguzo wa zamani ulikwisha muda wake mwaka 2014, akina mama walikuwa wanapata changamoto katika kutafuta mawakala wa vyandarua lakini utaratibu mpya ni kwamba mama mjamzito au mwenye mtoto mchanga atapewa chandarua chenye viuatilifu palepale atakapokuwa katika vituo vya kutolea huduma za afya ya uzazi” amesema.

Ameongeza kuwa mama atapewa chandarua katika hudhurio la kwanza la kliniki ambapo takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 98 ya wajawazito huhudhuria kliniki angalau mara moja pia vyandarua hivyo vitatolewa kwa idadi ya watoto ambao mama atakua amejifungua kwa wakati huo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza katika mkutano wa uelimishaji juu ya mpango endelevu wa ugawaji vyandarau vyenye viuatilifu vya mda mrefu uliofanyika Mkoani Singida.
Wajumbe wa mkutano wa uelimishaji juu ya mpango endelevu wa ugawaji vyandarau vyenye viuatilifu vya mda mrefu uliofanyika Mkoani Singida, wa kwanza ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi Pius Shija Luhende pembeni yake ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida Bravo Lyampembile.
Maafisa kutoka wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto wakiutambulisha mkoani Singida mpango endelevu wa ugawaji vyandarau vyenye viuatilifu vya mda mrefu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...