Naibu waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani amesema daraja la Mto
Momba lenye urefu wa mita 75 litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe litaanza
kujengwa mapema mwaka huu.
Eng. Ngonyani ametoa
kauli hiyo mara baada ya kukagua barabara ya Kasansa hadi Kilyamatundu na eneo
litakapojengwa daraja la Momba na kusema kuwa Serikali imeshampata Mkandarasi
atakajenga daraja hilo.
“Serikali imeshatoa
kiasi cha sh. Bilioni tatu fedha hizo
zimetusaidia kutangaza zabuni na kumpata mkandarasi, tayari Mkandarasi wa
ujenzi huu ameshapatikana na mkataba wa makubaliano ya ujenzi umeshakamilika
hivyo mkandarasi atausaini rasmi hivi karibuni,” amesema Eng. Ngonyani.
Aidha, Eng.Ngonyani
amemtaka Meneja Wa Wakala wa barabara (TANROADS) Mkoa wa Rukwa kuhakikisha
anatoa ajira kwa wakazi waliopo kata ya Kipeta ambapo ujenzi wa daraja hilo
utafanyika.
Naye Mbunge wa Jimbo
la Kwela Mhe. Ignas Malocha ameishukuru Serikali ya awamu ya tano ya Mhe. Dkt.
John Magufuli kwa kutekeleza ahadi ya ujenzi wa daraja hilo ambalo kukamilika
kwake kutawaletea maendeleo wakazi hao kwa vile litaufungua Mkoa wa Rukwa na
kuunganisha na Songwe na Katavi.
“Kukamilika kwa ujenzi
wa daraja hili kutarahisisha usafirishaji wa mazao ya biashara kutoka mkoa wetu
kwenda mikoa mingine inayopakana na mkoa huu na kuokoa maisha ya wananchi
ambapo awali walikuwa wa wakiliwa na mamba na wengine kusombwa na maji wakati
kuvuka kwenye mto huu,” amesisitiza Malocha.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akielekea kukagua
sehemu ambapo litajengwa Daraja la Momba litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na
Songwe .Kulia ni Meneja wa Wakala wa barabara
(TANROADS)Mkoa wa Rukwa Eng.
Msuka Mkina na Wa pili kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Kwela Mhe. Ignas Malocha.
Meneja
wa Wakala wa barabara(TANROADS), Mkoa wa Rukwa
Eng. Msuka Mkina (aliyenyoosha kidole) akimwonesha Naibu Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Wa tatu kulia) eneo
lipakapojengwa Daraja la Momba wakati alipokagua sehemu ambapo litajengwa
Daraja hilo litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe.
Muonekano
wa Sehemu ambapo daraja la Mto Momba litakapojengwa. Daraja hilo
litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Kulia) akitoa
maelezo kwa wananchi wa kijiji cha Kilyamatundu kata ya Kipeta Mkoani Rukwa
kuhusu ujenzi wa daraja la Mto Momba
litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe.
Wananchi
wa kijiji cha Kilyamatundu kata ya Kipeta Mkoani Rukwa wakifurahi mara baada ya
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (hayupo
picha) kutoa tamko la kupatikana kwa Mkandarasi atakayejenga daraja la Mto
Momba litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...