Saidi Mwamba Kizota (kushoto) na Hamisi Thobias Gaga |
Na Haji Sunday Manara
Ehhh!! Haya! Na leo naandika tena? Mazoea mengine bana!!
Ndio, nimeona niandike ujinga wangu ila safari hi naandika kuhusu suala jepesi la wachezaji kuhama timu kubwa moja kwenda timu kubwa nyingine. Hapa nazungumzia Simba na Yanga, aka mapacha Kulwa na Dotto.
Kiuhalisia hili jambo halikuanza leo,limeanza miaka Dahal. Na ukienda katika historia, zamani lilikuwa linakera zaid pengine kupita zama zetu, sababu miaka ya nyuma kabisa, wachezaji walikuwa wakihama upande mmoja kwenda mwingine sababu za kishabiki zaid kuliko sasa, ambapo sababu za kimaslahi zmechukua nafasi kubwa.
Kihistoria mchezaji wa kwanza maarufu kuhama katika timu hizi ni wajina wangu Haji Omari....Huyu alikuwa sentahafu mahiri sana wa Yanga, lakini akaja kuhamia Sunderland (Simba). Inaarifiwa kwa kitendo chake cha kuhama jinsi kilivyowakera wanayanga,wakaamua kuhakikisha hachezi Simba. Haji akaishia kuuza soda pale Ilala Stadium (Karume).
Baada ya hapo kulikuwa na mtikisiko mkubwa katika medani ya kabumbu nchini, baada ya anaetajwa kuwa kiungo bora nchini kuwahi kutokea miaka ya 19960 na mwanzoni mwa 1970 ,Gilbert Mahinya kuihama klabu ya Simba na kujiunga na Yanga. Kiungo huyo inatajwa kuwa alinyan'ganywa hadi fenicha alizonunuliwa na Simba,hali iliopelekea kuacha gumzo kubwa nchini. Gilbert anatajwa na mchezaji wa zamani wa Yanga, Pan, Pamba na timu ya Taifa,Mohamed Rishard Adoph, kuwa ndie half back six bora kuwahi kumuona nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...