Asasi za Kiraia za zinazounda
Umoja wa AZAKI za juu ya masuala ya Bunge kwa kushirikiana na asasi zingine waja
na mapendekezo katika kuboresha Sera ya Taifa ya Vijana ya mwaka 2007 ili
iendane na wakati pamoja na mabadiliko ya kiteknolojia.
Hayo yamebainishwa
leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Asasi ya Kiraia ya Dira ya Vijana
Tanzania (TYVA) ambayo ni Asasi kiongozi Bw. Suleiman Makwita wakati
akiwasilisha muhtasari wa uchambuzi wa Sera hiyo.
Makwita amesema kuwa
lengo la kufanya mapitio juu ya Sera hiyo ni kuangalia namma ambapo wanaweza
wakaishauri Serikali maeneo ya kufanyia maboresho katika Sera hiyo ya vijana.
“lengo la kufanya
uchambuzi huu ni kuiomba Serikali na wadau wote wa maendeleo ya vijan nchini
kuweka mazingira rafiki yatakayochochea maeneleo ya vijana kupitia sekta rasmi
na zisizo rasmi ikijuisha masuala mtambuka na kuendana na dhana ya maelengo
endelevu ya dunia” alisema Makwita.
Akizungumzia matokeo
ya uchambuzi huo Makweta alisema kuwa wamebaini baadhi ya changamoto zilizopo
katika Sera ya Vijana ya Mwaka 207 na hatimaye wamekuja na baadhi ya
mapendekezo kama njia ya kusaidia kuiboresha Sera hiyo.
Baadhi ya mapendekezo
waliyokuja nayo ni pamoja na kuanishwa kwa umri wa kijana kuwa miaka 13 -35
tofauti na sasa ambapo kijana anatambuli kuwa na umri kati ya 15 hadi 35.
Aliongeza kuwa katika
masuala ya afya Sera inapaswa kukugusia masuala yote yanayoathiri vijana kama
vile afya ya uzazi, anemia,TB na Selimundu, badala ya kutilia mkazo kwenye
VVU/Ukimwi pekee.
Pamoja na mapendekezo
hayo Makwita aliipongeza Serikali kwa juhudi zake za kuendelea kuweka mazingira
rafiki kwa vijana kijana, pamoja nakufanyia kazi baadhi ya mapendekezo ya wadau
mbalimbali ikiwemo kuanzishwa kwa Baraza la Taifa la Vijana.
Uchambuzi huu wa Sera
ya Taifa ya Vijana ya Mwaka 2007 umefanywa kwa ushirikiano baina ya umoja wa
AZAKI za Vijana juu ya Masuala ya Bunge na Mtandao wa AZAKI za Vijana juu ya
Masuala ya Afya ya Uzazi chini ya uongozi wa Asasi ya Dray a Vijana Tanzania
(TYVA).
Mwenyekiti wa Asasi ya Kiraia ya Dira ya Vijana
Tanzania (TYVA) Bw. Suleiman Makwita akiwasilisha muhtasari wa uchambuzi wa
Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya
mwaka 2007 mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) akiwa pamoja na baadhi
ya wananchama wa asasi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Asasi ya Kiraia ya Dira ya Vijana
Tanzania (TYVA) Bw. Suleiman Makwita akiwasilisha muhtasari wa uchambuzi wa
Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya
mwaka 2007 mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) akiwa pamoja na baadhi
ya wananchama wa asasi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Wanachama wa Asasi ya Kiraia ya Dira ya Vijana
Tanzania (TYVA) wakiwa katika pica ya pamoja mara baada ya kumaliza kuwasilisha
muhtasari wa uchambuzi wa Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 2007 kwa waandishi wa habari leo
Jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...