Shirika la MajiSafi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia wateja wake wote wa jiji la Dar-es-salaam, pamoja na Mji wa Kibaha Mkoani Pwani kuwa mtambo wa uzalishaji Maji wa Ruvu Juu utazimwa kwa wastani wa Saa 8, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni, siku ya Jumatatu tarehe 31/07/2017.

Sababu ya kuzimwa kwa Mtambo : Kumruhusu Mkandarasi (WABAG), kukamilisha Mfumo wa umeme katika mtambo mpya wa uzalishaji Maji wa Ruvu Juu uliopo Mlandizi mkoani Pwani.

Maeneo yatakayoathirika na Kuzimwa Kwa Mtambo huu:

Mlandizi Mjini, Ruvu Darajani, Vikuruti, Disunyara, Kilangalanga, Janga, Mbagala, Visiga, Maili 35, Zogowale, Misugusugu, Tanita, Kibondeni, Kwa Mathias, Nyumbu, Msangani, Kwa Mbonde, Picha Ya Ndege, Sofu, Lulanzi, Gogoni, Kibamba, Kibamba Njia Panda Shule Kibwegere, Mloganzira, Kwembe, Kibamba Hospitali, Kwa Mkinga, Luguruni, Kimara, Ubungo, na baadhi ya maeneo ya Tabata.

Toa taarifa Dawasco kupitia vituo vya wateja  Dawasco kimara 0743-451865, Dawasco Tabata 0743-451867, Dawasco Kibaha 0743-451875.

Dawasco inawaomba wateja kutunza Maji ya kutosha pindi Mtambo utakapokamilika
Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi: Kituo cha huduma Kwa wateja 0800110064 (BURE) au Tembelea: www.dawasco.go.tz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...