Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imezitaka hospitali nchini kutumia miongozo katika kutekeleza shughuli mbalimbali za huduma za afya  pamoja na kuimarisha mifumo ya TEHAMA ili kuwapo kwa mawasiliano kati ya Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na hospitali nyingine za rufaa nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa wizara hiyo Dk. Mpoki Ulisubisya wakati akizindua mpango wa kufuatilia utoaji wa huduma za afya yakiwamo mafanikio na changamoto katika hospitali za umma nchini.

Dk Ulisubisya amesema mpango wa wizara yake ni kuzitembelea hospitali za umma nchini utaanzia kwenye hospitali za kibingwa ili ziwe kitovu cha kutoa mafunzo kwa hospitali nyingine nchini.

“ Malalamiko ni mengi yanapaswa kushughulikiwa kwa kuwekwa mifumo imara ya utekelezaji wa shughuli za huduma za afya kwa lengo la kuzuia kushuka kwa ubora wa huduma. Pia, hali hii itasaidia kuimarisha maadili miongoni mwa watumishi,” amesema Dk Ulisubisya wakati akizindua mpango huo leo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubisya akizungumza katika mkutano wa kuzindua mpango wa kuzitembelea hospitali za umma nchini ili kujua mafanikio na changamoto zilizopo kwenye hospitali hizo. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru na Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tiba, Dk. Dorothy Gwajima wa wizara hiyo. Mpango huo umeandaliwa na wizara ya afya na ziara hiyo imeanza rasmi leo Muhimbili.
 Baadhi ya wataalamu wa afya kutoka Muhimbili na taasisi nyingine wakimsikiliza Katibu Mkuu, Dk Ulisubisya katika mkutano wa uzinduzi uliofanyika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
 Kaimu Mkurugenzi wa Tiba, Dk. Dorothy Gwajima (kushoto) wa wizara hiyo pamoja na wataalamu wengine wakifuatilia mkutano huo leo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza kabla ya kuzinduliwa kwa mpango wa kutembelea hospitali za umma ili kujua mafanikio na changamoto  zilizopo kwenye hospitali hizo.
 Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali, Dk Juma Mfinanga wa Muhimbili akimwelekeza jambo Kaimu Mkurugenzi wa Tiba, Dk. Dorothy Gwajima (kushoto) wa wizara ya Afya wakati wa ziara ya kutembelea hospitali hiyo leo. Wengine ni maofisa kutoka wizara ya afya na hospitali ya Muhimbili.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...