Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), Jeshi la Polisi kikosi cha Bandari pamoja na Jeshi la Uhamiaji wametakiwa kuhakikisha wanakagua abiria na mizigo yote inayopita katika bandari zote nchini ili kuhakikisha abiria na mizigo yote inafuata taratibu zote zilizowekwa kwa mujibu wa sheria jambo ambalo litaimarisha usalama bandarini. 
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masaun katika ziara ya kukagua namna watalii wanavyopokelewa katika bandari ya Dar es Salaam. 
Katika ziara hiyo aliambatana na Naibu Waziri wa Maliasili na utalii Mhandisi Ramo Makani na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi, na Mawasiliano Mhandisi Edwini Ngonyani. Kwa upande wake Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhandisi Ramo Makani amesema ni muhimu kuweka takwimu vizuri za watalii wanaopita katika bandari zote ili kujua idadi kamili ya watalii wanaokuja kwa kutumia njia ya maji. 
Akielezea jinsi wanavyowapokea watalii wanaokuja kwa meli katika bandari ya Dar Es Salaam, Meneja wa Operesheni amesema wamekuwa wakikutana na wadau kila siku ili kuhakikisha wanaweka mazingira mazuri ya ujio wa watalii nchini. Manaibu Waziri hao pia walitembelea Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal II na kukagua ujenzi wa Terminal III unaoendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...