Azam TV – Hotuba ya kwanza ya Rais mpya TFF Wallace Karia mjini Dodoma
Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini TFF umehitimishwa kwa aliyekuwa makamu wa Rais wa Shirikisho hilo Wallace Karia  (kulia) kushinda kwa jumla ya kura 95 na kuwabwaga wapinzani wake.
Uchaguzi huo umefanyika leo mkoani Dodoma ukiwa wa amani kwa wajumbe wa mkutano mkuu pamoja na wagombea wenyewe.
Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Revocatus Kuuli akitangaza matokeo hayo ambapo alimtangaza Wallace Karia kama mshindi wa kinyang'anyiro kwa kura 95 kati ya kura 127 zilizopigwa.
Wagombea Urais wa TFF na kura zao ni: Emmanuel Kimbe (1). Frederick Mwakalebela (3), Imani Madega (8), Richard Shija (9)  Ally Mayai  (9) na Wallace Karia  (95).
Kuuli ametangaza kuwa, katika nafasi ya makamu wa Rais, Michael Richard Wambura (kushoto) ameshinda nafasi hiyo kwa kura 85.
Kwa upande wa wajumbe wa mkutano mkuu kumekuwa na maingizo mapya kutoka kanda mbalimbali za nchini kama ifuatavyo:
Zone 1: Saloum Chama 
Zone 2: Vedastus Lufano 
Zone 3: Mbasha Matutu 
Zone 4: Sarah Chao 
Zone 5: Issa Bukuku 
          Zone 6: Kenneth Pesambili 
Zone 7: Elias Mwanjala 
Zone 8: James Mhagama 
Zone 9: Dunstan Mkundi 
                                                    Zone 10: Mohamed Aden 
                                                 Zone 11: Francis Ndulane 
                                              Zone 12: Khalid Abdallah 
                                                 Zone 13: Lameck Nyambaya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...