Chama Cha Mapinduzi(CCM)wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma kimewakutanisha viongozi wa serikali na wa Chama ngazi ya Tarafa katika semina ya siku moja lengo likiwa ni kuwapa uelewa wa pamoja wakati wa  kutekeleza majukumu yao ya kazi.

Akifungua semina hiyo katika kata ya Nzoisa wilayani Kongwa Katibu CCM mkoa wa Dodoma Jamila Yusuph  amewataka viongozi hao kufanya kazi kwa pamoja ili kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama hicho kama ilivyoahidiwa.

Ili hilo litekelezeke amewaasa kujenga umoja na maelewano katika sehemu zao za kazi kwa kuelezana ukweli pale wanapoona kuna jambo haliendi sawa na kutatua kero za wananchi kama walivyoahidi.

Alisema viongozi wa Chama na Serikali wakiwa tofauti ilhali kazi ya kupeleka maendeleo kwa wananchi kutokana na Ilani iliyopo inapaswa kufanya kwa ushirikiano wanakuwa wanawakosea wananchi walioichagua CCM na kuiweka madarakani.
 PICHA (1)
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Deogratius Ndejembi akizungumza na viongozi wa Chama na Serikali wa Tarafa ya Nzoisa wilayani humo katika semina ya kujenga uelewa wa namna ya kutekeleza majukumu yao kwa pamoja.
PICHA (2)
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)mkoa wa Dodoma Jamila Yusuph akifungua semina hiyo kwa viongozi wa chama na serikali ngazi ya Tarafa ambapo amesisitiza ushirikiano,upendo na umoja katika kuitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM iliyopo.
PICHA (4)
Katibu wa CCM mkoa wa Dodoma akiongoza viongozi wa Chama na Serikali wa wilaya ya Kongwa kuimba wimbo wa Chama katika semina hiyo,miongoni mwa viongozi hao yupo mkuu wa wilaya hiyo Deogratius Ndejembi,katibu wa CCM wilaya Mfaume Kizigo na mwenyekiti wa halmashauri White Zubeir.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...