Na Felix Mwagara (MOHA)
MWENYEKITI wa Baraza la
Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema Baraza lake litakutana kujadili uwezekano
wa Jeshi la Polisi, Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) pamoja na Chuo cha
Usafirishaji (NIT) ziweze kuungana ili kufanya ukaguzi wa lazima wa magari kwa
lengo la kuondoa ajali nchini.
Akizungumza jijini Dar
es Salaam jana mara baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea ofisi za Temesa
na Chuo cha NIT, Masauni alisema ziara yake ilikua na mafanikio makubwa, hivyo anatarajia
kukutana na Wajumbe wa Baraza lake katika vikao vyao na kuwasilisha uzoefu
alioupata mara baada ya kuzitembelea Taasisi hizo za Serikali.
“Nimeshuhudia Temesa na
NIT mambo ambayo sikuyatarajia, inaonyesha kwamba katika vita ya kuzuia ajali
nchini hatutaanza sifuri, tunasehemu fulani ya kuanzia, tutaanza na utaratibu
wenye mfumo mzuri ambao utaweza kutekelezwa ili kufikia malengo ya kuwa na
utaratibu wa lazima wa ukaguzi wa magari yote ambayo yanatumika katika nchi
yetu,” alisema Masauni na kuongeza;
“Lengo la mipango hiyo
ni kuhakikisha tunakuwa na magari mazuri ambayo hayawezi kusababisha ajali,
hivyo nitawasilisha katika kikao hicho chha Baraza uzoefu huu nilioupata baada ya
ziara hii ili nijadiliane na wajumbe wenzangu tuone jinsi tutakavyokubaliana
kuhusiana na mafanikio niliyoyapata baada ya ziara hii.”
Mwenyekiti
wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akiwa na Mtendaji Mkuu wa
Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu (kushoto) na Mkurugenzi wa
Uzalishaji na Matengenezo Temesa, Mhandisi Sylvester Simfukwe (kulia), wakati
Mwenyekiti huyo alipokuwa anatoka kuiangalia Karakana ya Utengenezaji wa Magari
iliyopo katika ofisi za Temesa, Keko, jijini Dar es Salaam. Masauni alisema
lengo kubwa la ziara yake, kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza
kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili
kukabiliana ajali za barabarani nchini.
Mwenyekiti
wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (aliyekaa), akimsikiliza rubani Edger
Mcha (kulia) wa Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT) kilichopo jijini Dar es
Salaam, wakati alipokua anamuonyesha jinsi ya kuongoza ndege inapotaka kuruka na
kutua kutoka katika kiwanja cha ndege. Mwenyekiti huyo alipata maelezo hayo
wakati alipokua katika darasa la kufundishia marubani chuoni hapo. Masauni
alifanya ziara katika chuo hicho na Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), kwa
lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa
Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za
barabarani nchini. Akiwa chuoni hapo aliangalia ukaguzi wa magari na pia kupata
mipango mbalimbali waliyonayo kuhusiana na elimu wanayoitoa ya kuhusiana na
usalama barabarani. Aliyevaa koti ni Mkuu wa Chuo hicho, ambaye pia ni Mjumbe
wa Baraza hilo, Profesa Zakaria Mganilwa.
Mwenyekiti
wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akiangalia mashine ya
kukagua magari kwa njia ya umeme iliyokua inaonyeshwa na Mhandisi Yakubu Kibingo
wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA. Katikati ni Meneja wa Karakana ya
kutengeneza magari na mitambo mbalimbali ya Serikali, Julius Humbe. Masauni alifanya
ziara katika ofisi hiyo iliyopo Keko, jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kuangalia
jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati
iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za barabarani nchini.
Mwenyekiti
wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Chuo
cha Usafirishaji nchini (NIT), Profesa Zakaria Mganilwa (katikati) alipokua anatoa
historia ya chuo hicho pamoja na kozi mbalimbali zinazofundishwa katika chuo
hicho, kilichopo Mabibo jijini Dar es Salaam. Masauni alifanya ziara chuoni
hapo kwa lengo la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha
Utekelezaji wa Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana
ajali za barabarani nchini. Kulia ni Naibu Mkuu wa Chuo hicho kwa upande wa Taaluma
Utafiti na Ushauri, Dk. Prosper Mgaya.
Mkuu wa Idara ya Teknolojia
ya Usafirishaji wa Chuo cha Usafirishaji nchini (NIT), kilichopo Mabibo, jijini
Dar es Salaam, Amon Mwasandube, akimuonyesha Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la
Usalama Barabarani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni (katikati), jinsi gari linavyokaguliwa linapokuja katika Kituo
cha Ukaguzi wa Magari chuoni hapo. Masauni alifanya ziara chuoni hapo kwa lengo
la kuangalia jinsi gani Baraza lake linaweza kufanikisha Utekelezaji wa
Mapendezo ya Kamati iliyoundwa na Baraza hilo ili kukabiliana ajali za
barabarani nchini. Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Zakaria Mganilwa. Picha
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...