NA
K-VIS BLOG/Khalfan Said.
BINADAMU
ili aweze kuyakabili mazingira yake, moja ya nyenzo muhimu ni elimu, na kwa
kutambua umuhimu wa elimu, wadau mbalimbali wamekuwa wakifanya juhudi kubwa
katika kusaidiana na serikali ili kufikia lengo la kuwapatia elimu Wananchi wa
Tanzania.
Mtandao
wa Elimu Tanzania, kwa kifupi TenMet, ni moja ya taasisi zinazifanywa juhudi
kub wa katika kuhakikisha malengo yaliyotajwa hapo juu yanafikiwa.
TenMet
ambayo iliasisiwa miaka 18 iliyopita ikiunganisha taasisi nyingine 39 wakati
huo, kwa sasa mtandao huo umepanuka na kufikia jumla ya taasisi 181
zilizojikita katika swala la kuhakikisha watanzania wanapatiwa haki yao ya
elimu, lakini sio tu kupatiwa elimu bali pia elimu iliyo bora.
Ili
kufikisha ujumbe kwa wahusika (jamii) TenMet hufikisha ujumbe kwa njia mbalimbali
ikiwa ni pamoja na makongamano, semina na vyombo vya habari vikiwemo vile vya
kisasa (social media kama vile Blogs).
Agosti
2, 2017, Maafisa wa TenMet waliwaalika bloggers ili kuangalia namna gani
wanavyoweza kushirikiana katika kutekeleza malengo yaliyoanishwa hapo juu ya
kusambaza taarifa mbalimbali zinazohusu masuala ya elimu.
Akizungumza
kwenye mkutano huo, Meneja Programu wa TenMet, Bw.Nicodemus Shauri Eatlawe, alisema,
lengo la mkutano huo ni kuimarisha ushirikiano wa kikazi baina ya taasisi yake
na vyombo vya habari vya kimtandao kwani anaamini taarifa zitawafikia wadau
wengi zaidi.
“Lakini
pia tunaamini ushirikiano huu utatusaidia katika kuibua changamoto mbalimbali
zinazoikabili sekta ya elimu nchini, kwa kuhabarisha umma, hivyo tunayo furaha
kubwa kukutana nanyi leo hii.”Alifafanua.
Kwa
upande wake, Afisa Programu wa TenMet, Bi. Alistidia Kamugisha, amefafanua
kuwa, TenMet kama ambavyo malengo yake yalivyoainishwa, imekuwa ikifanya tafiti
mbalimbali kuhusu elimu hapa nchini, lakini pia kwa kushirikiana na taassi
nyingine za kimataifa ikiwa ni pamoja na kuratibu mikutano, maonesho na semina kuhusu
masuala ya elimu.
Afisa
Programu wa Mtandao wa Elimu Tanzania, (TenMet), Bi. Alistidia
Kamugisha, akizungumza wakati wa kikao cha kujenga ushirikiano baina ya
taasisi hiyo na Bloggers kilichofanyika makao makuu ya TenMet, Sinza
jijini Dar es Salaam, leo Agosti 2, 2017.
Meneja
Programu wa TenMet, Bw.Nicodemus Shauri Eatlawe, (katikati), akifafanua
jambo wakati wa kikao hicho. Kulia ni Bi. Alistidia Kamugisha, na Afisa
Programu wa taasisi hiyo, Bw. David Sizya.
Afisa wa TenMet, Bw. Dominic Dogani, akitoa ufafanuaiz wa masuala mbalimbali yatakayojadiliwa kwenye kikao hicho.
Majadiliano yakiendelea..
Bw. Sizya, (kulia), akimpatia nakala ya vitabu vya TenMet mwandishi wa Mo Blog, Bw. Rabif Humwe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...