Halmashauri
ya Mji wa Kibaha Mkoani Pwani ,imesitisha zuio la kuingiza na kufanya
biashara ya nguruwe na mazao yake ,:"ambapo juni mwaka huu ilipiga
marufuku biashara hiyo ili kuepuka na ugonjwa wa homa ya
nguruwe(AFRICAN SWINE FEVER) .
Halmashauri
hiyo ilichukua hatua hiyo kutokana na idara ya mifugo na uvuvi kubaini
kuingia kwa ugonjwa huo katika baadhi ya maeneo .
Akizungumzia suala hilo ofisini kwake mjini humo,ofisa habari wa halmashauri ya mji wa Kibaha,Innocent Byarugaba,alisema idara hiyo imefanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa hakuna tena viashiria hivyo na kuamua kusitisha zuio hilo.
Aidha alieleza jumla ya nguruwe 71 wenye thamani ya sh.mil.4.970 walikufa kutokana na ugonjwa wa homa ya nguruwe.
Kwa
mujibu wa Byarugaba ,uwepo wa kuzuia na kusitisha kipindi hicho
kulisaidia kupunguza na hatimae kudhibiti ongezeko na kuenea kwa ugonjwa
huo .
"Halmashauri hii
kuanzia sasa inapenda kuutarifu umma kuendelea na shughuli zake kama
kawaida na kwamba zuio limeondolewa rasmi "alisema Byarugaba.
Alieleza
sababu iliyosababisha kupigwa marufuku kuingia mnyama huyo na kuathiri
hasa wauza kitimoto kwamba ni ugonjwa wa homa ya nguruwe kuingia kwenye
kata mbili za Picha ya Ndege na Viziwaziwa eneo la Mikongeni.
Nae
Afisa mifugo na uvivu wa halmashauri ya mji wa Kibaha, Charles Marwa
,alisema hatua za awali zilizochukuliwa ikiwemo kuzuia nguruwe kuingia
na kutoka katika maeneo yaliyokuwa na viasharia.
"Sampuli
mbalimbali za nguruwe waliokufa zilichukuliwa na kupelekwa maabara kuu
ya mifugo Temeke Jijini Dar es Salaam kwa uchunguzi na kubaini uwepo wa
ugonjwa huo ,” alisema Marwa.
Marwa
alibainisha ,ugonjwa wa African Swine Fever,ambao unadaiwa kuingia
kwa nguruwe hauwezi kuambukiza binadamu ila madhara yake makubwa ni
kuteketeza nguruwe wengi asilimia 100,kwa muda mfupi na kusababisha
hasara kwa mfugaji.
Alitaja
dalili za ugonjwa huo ni kuvuja na kusambaa kwa damu kwenye viungo vya
mwili , homa kali, kupumua kwa shida na, kutapika.
Vifo ndani ya siku mbili hadi 10 na muonekano wa damu kuvilia kwenye viungo mbalimbali vya ndani vya nguruwe baada ya kumpasua.
Ugonjwa
huo hushambulia nguruwe na hauna tiba kwa wanyama wanaoupata na
husababisha vifo vingi unapotokea hasa kwa wanyama wakubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...