Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linashiriki maonyesho ya Kilimo yanayoendelea mkoani Morogoro, Katika maonyesho hayo wakazi wote wa Morogoro Hususan Wakulima wanakaribishwa kupata elimu kuhusu namna ya kushiriki kilimo cha miwa (Outgrowers Scheme) Mpango huu umeanziishwa mahususi ili kuwasaidia watanzania kupata kipato kwa kulima miwa na Miwa hiyo itanunuliwa moja kwa moja na Kampuni Hodhi ya Mkulazi ambayo ni ubia kati ya NSSF na PPF. 

Vile vile wananchi wote wanakaribishwa kujiandikisha na NSSF ili kupata Matibabu bure kwa mwanachama na wategemezi wake pamoja na Mafao mengine yatolewayo na NSSF kama vile Mafao ya uzazi, kuumia kazini, Mafao ya urithi, Pensheni ya uzeeni na mengineyo
Afisa wa NSSF Mr Shaban Salehe akimwandikisha mwanachama mpya katika banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.
Afisa wa NSSF, Mwanawetu Njozi (kulia) akiongea na mgeni alietembelea banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.
Afisa wa NSSF, Jonathan Mkahala akimwandikisha mwanachama mpya katika banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro, Pembeni kushoto ni Afisa mwandamizi wa Matekelezo wa Shirika hilo, Bw. Salawa.
Afisa Mwandamizi wa Masoko na Uhusiano, Amina Mbaga akizungumza na wageni walietembelea banda la NSSF katika maonyesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...