Waziri Wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (Katikati), akizungumza na wafanyabiashara
wanaotoa huduma katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere
(JNIA), wakati alipofanya kikao cha pamoja, leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri Wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Kaimu
MKurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Salim
Msangi (Kulia), wakati alipokagua sehemu ya kuingilia abiria katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), leo jijini Dar es Salaam.
Waziri Wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akizungumza na wafanyabiashara
wanaotoa huduma katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere
(JNIA), wakati alipofanya kikao cha pamoja, leo Jijini Dar es Salaam.
Picha
na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ametoa Mwezi mmoja kwa wafanyabiashara wanaotoa huduma katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) kulipa kodi ya Majengo kama mikataba yao inavyolekeza.
Waziri Mbarawa ametoa agizo hilo leo wakati alipokutana na wafanyabiashara hao ili kujadili changamoto mbalimbali zilizopo na jinsi ya kuzitatua ili kuendelea kutoa huduma bora katika uwanja huo.
“Kulipa kodi za majengo hapa ni suala la lazima, hivyo ifikapo Septemba mwishoni nataka kuona wafanyabiaashara wote mmeshalipa kodi ya pango, makusanyo haya ni muhimu kwetu ili tuendelee na hatua nyingine za uboreshaji wa viwanja vya ndege na huduma nyinginezo.” Amesisitiza Profesa Mbarawa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...