Mkurugenzi Mwendeshaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), Ladislaus Matindi, akizungumza na waandishi wa habari, wakati akielezea kuhusu makubaliano ya ushirikiano ya kutoa huduma na Shirika la Posta Tanzania (TPC), jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Postamasta Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa. Makubaliano kati ya taasisi hizo, ni katika nyanja za 1. Usafirishaji wafanyakazi, wanaposafiri kikazi, 2.Usafirishaji wa mizigo, vifurushi na barua kupitia ndege za ATCL, 3. Kubadilishana uzoefu wa namna ya kuhudumia wateja, 4. Ushirikiano wa matumizi ya majengo ya Ofisi na 5. Kushirikishana kwenye tovuti kuhusu mambo yote ya Masoko.
Postamasta Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa (kulia) na Mkurugenzi Mwendeshaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi (kushoto), wakitia saini mkataba huo wa ushirikiano kati ya taasisi zao hizo. Kulia anayemsaidia Postamasta Mkuu ni Mwanasheria wa TPC, Bi. Zuhura Pinde.
Postamasta Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa (kushoto) na Mkurugenzi Mwendeshaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi (kulia), wakiuonesha kwa waandishi wa habari mkataba huo, mara baada ya kuusaini jijini Dar es Salaam leo.   
Postamasta Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa (kulia) akimtambulisha baadhi ya watendaji wa shirika hilo, Mkurugenzi Mwendeshaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi (wa pili kulia), mara baada ya kumalizika shughuli hiyo, Dar es Salaam leo.  



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...