Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Bw.Ramadhani Kaswa, ameipongeza na kuishukuru Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA kwa huduma nzuri kwa wananchi wa Lindi na mkoa jirani wa Mtwara ambao wameendelea kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa katika siku za maonyesho ya Nanenane Kitaifa yanayofanyika kwa mara ya nne mfululizo mkoani humo.
Mbali na kupongeza kazi kubwa inayofanywa na NIDA, Katibu Tawala huyo amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kusajiliwa kwani ni fursa muhimu ya kupata Vitambulisho vya Taifa kwa wakati.
“ Wananchi jitokezeni kwa wingi ili msajiliwe; hii ni fursa muhimu kwenu. NIDA hongereni sana na naomba muendelee na ari hiyo ya  kuwahudumia wananchi” alisisitiza
Mamia ya wananchi wamejitokeza kwa wingi kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane Kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi, sambamba na kujifunza ukulima wa kisasa.
Wananchi mbali na kusajiliwa; huduma nyingine zinazotolewa kwenye banda la NIDA; ni Ugawaji wa Vitambulisho kwa wananchi waliokamilisha taratibu za Usajili, kutoa taarifa za hatua ya uzalishaji Vitambulisho kwa wananchi ambao walishasajiliwa awali na hawajapata Vitambulisho vyao, pamoja na kupata elimu ya jumla kuhusu Vitambulisho vya Taifa, faida na matumizi.
Kupia fursa hii wananchi wanaosajiliwa wameahidiwa kupata Vitambulisho vyao ndani ya mwezi mmoja ili kutoa fursa ya uhakiki wa taarifa na uzalishaji.
 
 Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Bw. Deodatus Alexander akimkabidhi kitambulisho chake Bw. Abrahman Mohamed Mussa, akiwa miongoni mwa wananchi waliokamilisha taratibu za Usajili na kukabidhiwa Vitambulisho vyao wakati wa maonyesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya Ngongo Lindi.
 Baadhi ya wananchi wakikamilisha taratibu za Usajili kwa kuchukuliwa alama za vidole, picha na saini ya Kielektroniki wakati wa maonyesho yanayoendelea Viwanja vya Ngongo Lindi.
 Wananchi wa Manispaa ya Lindi wakipata maelezo ya taratibu za Usajili toka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi.Rose Mdami wakati maonyesho ya Nanenane yakiendelea mkoani Lindi.
 Wananchi wakiendelea kusubiria kupata huduma ya Usajili kwenye banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) mkoani Lindi.

 Bi Khadija Khalid mtaalamu wa mifumo ya Komputa mkoani ofisi ya NIDA Lindi, akitoa elimu kuhusu mfumo wa Utambuzi na Usajili wa Taifa kwa wananchi waliofika kujifunza kwenye Banda la NIDA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...