Wasanii wa Bongo Freva  hapa nchini wameaswa kuzingatia matumizi ya Lugha pamoja na mavazi  ili kuepusha fungia fungia ya kazi zao za sanaa.

Hayo yamesemwa leo wakati wa mkutano wa  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe na wasanii wa nyimbo za bongo Freva pamoja na wadau mbalimbali na sanaa hapa nchini jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na wasanii wa nyimbo za Bongo Freva hapa nchini kuhusu maswala mbalimbali yanayowahusu wasanii hao, pia wameshauliwa kujiunga kusajili kazi zao pamoja na kulipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kupata miongozo mbali mbali COSOTA pamoja na BASATA.
 Baadhi ya wasanii wa Nyimbo za Bongo Freva  hapanchini kutoka kulia ni Wastara Thomasi, msanii wa Bongo Fleva, Khadija Shaban (Keisha) na Witnes Mwajaga wakiwa katika Mkutano wa wasanii wa Bongo freva na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe jijini Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe akipokea saa ya ukutani ikiwa ni Rambirambi kutoka kwa wasanii wa Mziki wa Bongo Freva  kama pole kufiwa na Mkewe.
                   Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii. 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...