NMB Bank imeendesha mafunzo kwa wajasiriamali zaidi ya 600 wa Iringa mjini na
wilayani Mafinga yenye lengo la kuwapa ujuzi wa jinsi ya kukuza biashara zao kwa
maendeleo ya kiuchumi nchini.
Wafanyabiashara hao walipewa mafunzo yanayohusu bidhaa zinazotolewa na NMB
kama jinsi ya kutunza vitabu vya mahesabu, elimu ya masoko na pia elimu ya
mlipa kodi na matumizi bora ya mikopo wanayopatiwa na benki ya NMB.
Akizungumza kwenye mkutano wa wafanyabiashara zaidi ya 300 wa mjini Iringa,
Meneja Mahusiano ya Wateja wa NMB, Wogofya Mpafalamagoa alisema kuwa
katika kuwajaliWateja wake wadogo na wakati, NMB imekuwaikiendesha
mafunzo ya wajasiliamali nchi nzima ili kuwapa elimu ya jinsi ya kukuza biashara
zao.
“kuna wafanyabiashara hapa wameanza na mitaji midogosana, wameanza kwa
kukopa shilingi laki 5 tu na kuziwekeza kwenye biashara, kupitia mafunzo haya na
pia ushauri tunaowapa, wamekuza mitaji yao na wengine sasa wanakopa
mabilioni NMB.” Alisema Mpafalamagoa.
Mafunzo hayo ya wajasiliamali yalifanyikakwa klabu za biashara za Iringa mjini na
Wilayani Mafinga ambapo zaidi ya wafanyabiashara 600 walihudhuria na
kunufaika na mafunzo kutoka NMB.
Meneja Mahusiano ya Wateja wa NMB – Wogofya Mpafalamagoa akitoa mada kwenye mkutano wa wajasiliamali uliondaliwa na benki ya NMB. Zaidi ya wafanyabiashara zaidi ya 300 wa wilayani Mafinga walihudhuria mkutano huo ambapo pia walipewa mafunzo ya jinsi ya kukuza biashara zao.
NMB ina business club 34 nchi nzima zenye wanachama zaidi ya 10,000 ambao
wamekuwa wakifaidika na mafunzo mbalimbali kutoka NMB yanayohusu
bidhaa zinazotolewa kwao na benki kama jinsi ya kutunza vitabu vya mahesabu,
elimu ya masoko na pia elimu ya mlipa kodi. Mpafalamagoa alisisitiza kwamba lengo kugawa vilabu hivyo vya biashara
vimeundwa kuhakikisha wafanyabiashara nchini wanakuza mitaji yao,
kuajiri watanzania wengi zaidi na pia kuchangia uchumi wa taifa hili kupitia ulipaji
kodi.
Mpafalamagoa aliongeza kuwa ilikuhakikisha benki hiyo inachangia ukuaji wa
sekta ya biashara nchini, imeanzisha vilabu vya wafanyabiashara (NMB Business
Clubs) ambao ndio walengwa wa vituo vya biashara.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mafinga, Daniel Mwasela aliwataka wafanya biashara wa
wilaya ya Mufindi kujengaurafiki wa karibu na benki ya NMB Ili waweze kukuza
biashara zao kupitia mikopo ya ainambalimbali ambapo yoteinalengakumkwamua
kiuchumi mjasiliamali.
Wafanyabiashara wadogo na wakati wanawakilisha asilimia 14 ya biashara ya
NMB. NMB imeanza kufanya jitihada mbalimbali kuhakikisha kuwa wanachama
wake wanafikia idadi ya 25,000 kufikia mwishoni mwamwaka2017.
Wanachama wa klabu ya Biashara (NMB Business club) niwajasiliamaliambao
wamekuwa wakiwezeshwa mara kwa mara na benki kwaajili ya kuendeleza
biashara zao. Nje ya mafunzo na vituo hivisitavya wafanyabiashara,
Wajasiriamalihawawanapatafaida ya kutumia mtandaompana zaidi wa matawi
zaidi ya 200 ya NMB na ATM zaidi ya 700 nchi nzima.
Sehemu ya Wajasiliamali wadogo wakiwa kwenye mkutano wa klabu ya Biashara mjini Iriga juzi. Zaidi ya wafanyabiashara zaidi ya 300 wa wilayani Mafinga walihudhuria mkutano huo ambapo pia walipewa mafunzo ya jinsi ya kukuza biashara zao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...