SERIKALI imesema kuwa ipo tayari kuingia kugharama zozote ili kumpeleka kwenye matibabu mahali popote duniani Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Tundu Lissu iwapo watapokea maombi kutoka kwa ndugu na familia yatakaothibitishwa na daktari kuwa anahitaji huduma ya madaktari wa bingwa zaidi.

Akitaka apelekwe Marekani,Ujerumani na mahali mengine ikiwemo India tunaweza kumpeleka iwapo watapeleka maombi kwa serikali kutaka ifanye hivyo ili  kuhakikisha anapata matibabu stahiki. 

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Tanga ambapo alisema wakipita maombi watatekeleza suala hilo haraka iwezekanavyo.

"Serikali haitakataa wala kushindwa kumuhudumia Tindu Lissu yeye ni Mtanzania kama wanavyohudumiwa wengine hivyo wao wapo tayari kuhakikisha anapata matibabu bora nje ya nchi "Alisema .Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga wakati akitangaza kuwa serikali ipo tayari kumpeleka kwenye matibabu mahali popote duniani mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Tundu Lisu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...