Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Exim Tanzania, Dinesh Arora akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Hon Halima Dendego vitanda na magodoro 40 venye thamani ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya hospital ya rufaa ya Ligula mjini humo kama sehemu ya kampeni yake yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya kutumikia jamii, Mganga Mkuu wa Mkoa Dr.Wedson Sichalwe.

Wafanyakazi wa benki ya Exim wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa hospitali ya rufaa ya Ligula mjini.

BENKI ya Exim Tanzania imekabidhi vitanda na magodoro 40 yenye thamani ya TZS 20M / - kwa Hospitali ya mkoa iliyoko Mtwara, kama sehemu ya kampeni yake yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya kutumikia jamii.

Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma, mwezi wa Agosti mwaka huu,kwakuzindua mradi wa mwaka mzima unaoitwa “miaka 20 ya kujalijamii”ambao Benki hiyo itawekeza shilingi milioni 200 katika sekta ya afya Tanzania.

Mradi huu unalenga kusaidia upungufu wa vitanda katika hospitali nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro na vitanda 500 katika hospitali za serikali katika mikoa 13 nchini.

Hospitaliyamkoa, Mtwara, nihospitaliyatatukupokeamchangohuu, baadayaHospitaliyaMnaziMmoja, Unguja, Zanzibar mweziuliopita. TukiolilifanyikakwenyehospitalihiyonamgenirasmialikwaMkuuwamkoa Halima Dendego.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya Exim, Stanley Kafualisema, “ Mwaka huu benki ya Exim imefikia hatua muhimu sana. 
Tunasheherekea miaka 20 ya uvumbuzi na kujitolea kwajamii. Kwa miaka mingi benki ya Exim imewekeza kwa kiasi kikubwa katika sekta ya afya, mazingira na elimu nchini.
Tunatambua juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya hivyo basi tumejitolea mwaka huu mzima kuwekeza katika hospitali za serikali katika maeneo mbalimbali nchini.” 

Hospitali na kliniki nyingi nchini zinatatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa. Takwimu za Shirika la afya duniani ‘WHO’ zinaonyesha kuwa Tanzania ina uwiano wa vitanda saba kwa kila watu elfu kumi. Hivi sasa hali ya kuona wakina mamawajawazito wawili wa kitumia kitanda kimoja au wengine  kulala sakafuni ni jambo la kawaida katika hospitali hizi. 

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego alipongeza Exim Bank Tanzania kwa ahadi yake ya kukabiliana na upungufu wa  vitanda kwenye hospitali ambao unakabiliwa na taifa na kuleta juhudi zake kwa hospitali ya  Mkoa wa Mtwara.

Afisa wa matibabu wa Hospitali ya mkoa,Mtwara alisema“Upungufu wa vitanda katika hospitali ni changamoto kubwa. Msaada huu kutoka benki ya Exim wahivi vitanda 40 na magodoro utasaidia sana katika kupunguza changamoto hii.”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...