Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na uvuvi Mhe.Abdalla Hamisi Ulega amefanya ziara mkoani Arusha katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kwa lengo la kuhamasisha upigaji chapa mifugo.

Akizungumza na baadhi ya wafugaji katika halmashauri ya Ngorongoro, Ulega amempongeza mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo, kwa utendaji mzuri wa kazi hususani katika kuhamasisha upigaji chapa mifugo mkoani humo.

Aidha Mhe Ulega amezijata baadhi ya halmashauri zilizofanya vizuri katika zoezi la upigaji chapa kuwa ni pamoja na Chemba,Kondoa,Maswa,Mafinga na Misungwi.

Mh.Ulega amewahimiza wafugaji kujitokeza kwa wingi katika zoezi la upigaji chapa mifugo linaloendelea nchi zima.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akishiriki zoezi la upigaji chapa mifugo katika hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha.
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akizindua zowezi la upigaji chapa mifugo katika hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, (wa kwanza kulia) akizungumza na wananchi wanoishi katika hifadhi ya Ngorongoro jana baada ya kushuhudia zowezi la upigaji chapa mifugo mkoa wa Arusha.katikati ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na kushoto, Naibu Muhifadhi Dkt.Maurus Msuha
Naibu Muhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro,Dkt Maurus Msuha  akishiriki zowezi la upigaji chapa mifugo mapema jana mkoani Arusha.

Zowezi la upigaji chapa mifugo likiendelea mkoani Arusha.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG Arusha)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...