Shindano hilo ambalo lililokuwa linashirikisha vijiji 33 kutokea wiayani humo, limehudhuriwa na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa jimbo hilo Mheshimiwa Jumaa Hamidu Awesso ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi.

Awali akitangaza kamati tatu bora zilizofanya vizuri kwa mwaka huu mbele ya mgeni rasmi, mkurugenzi msaidizi kutokea shirika la UZIKWASA Bwana Novatus Urassa alisema, mchakato wa kupata washindi hao ulikuwa mgumu kwa kuwa mwaka huu kamati zote zilionesha ushindani wa hali ya juu katika kutekeleza mipango kazi yao waliyojiwekea.

"Mheshimiwa mgeni rasmi, takribani vijiji vyote 33 vilivyoshiriki shindano hili kwa mwaka huu vilikuwa moto, kwa maana kila kijiji kilikuwa na mpango kazi wake, na kwa asilimia kubwa wote wamefanikiwa kutekeleza mipango kazi hiyo, lakini wapo waliotekeleza vizuri zaidi na tukaona hao ndio watakuwa mfano mzuri kwa wenzao, hivyo mpaka kupata kumia (10) bora haikuwa kazi rahisi, hivyo hivyo mpaka kupata hizi tatu (3) bora pia haikuwa rahisi" alisema Bwana Urassa.

Bwana Urassa alizitaja kamati hizo zilizofanya vizuri kuwa ni kamati ya kijiji cha Msaraza ambacho ndicho kiliibuka na ushindi na kukabidhiwa zawadi ya hundi ya shilingi laki saba, mshindi wa pili ni kijiji cha Mwera ambacho kilipewa hundi ya shilingi laki sita na mshindi wa tatu ni kijiji cha Mkwajuni ambapo walikabidhiwa hundi ya shilingi laki tano.

Mheshimiwa Naibu waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Hamidu Awesso akitoa ngao ya ushindi kwa mjumbe wa kamati ya kudhibiti Ukimwi, Jinsia na Uongozi ya kijiji cha Msaraza wakati wa tamasha hilo

Mheshimiwa Naibu waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Hamidu Awesso akitoa zawadi kwa kijana bora wa mfano wa kuigwa kwa mwaka 2017 nafasi ya kwanza ilichukuliwa na kijana Selemani Hamisi kutokea kijiji cha Kimang'a(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

Mheshimiwa Naibu waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Hamidu Awesso akitoa zawadi kwa mama bora wa mfano kwa mwaka 2017 ambapo nafasi ya kwanza ilikwenda kwa Mama Hadija Mrisho wa kijiji cha Kwa-Kibuyu pichani

Hatimae shindano la kutafuta kamati bora za kudhibiti Ukimwi, Jinsia na Uongozi vijijini lililokuwa linaratibiwa na shirika la UZIKWASA wilayani Pangani limemaliza kwa kishindo huku kamati ya kijiji cha Msaraza kikiibuka na ushindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...