Na Emmanuel Ghula
WADAU
wa Takwimu nchini wamekutana ili kujadili upatikanaji wa Takwimu za
msingi na uzalishaji wa takwimu na mapungufu yaliyopo katika kupima na
kufuatilia utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya Kitaifa, Kikanda na
Kimataifa.
Akizungumza
wakati akifungua warsha ya siku mbili ya wadau hao, Naibu Katibu
Mtendaji Tume ya Mipango, Wizara ya Fedha na Mipango Mhandisi Happiness
Mgalula amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa
Maendeleo pamoja na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wameandaa warsha
hiyo ili kujadili namna bora ya upatikanaji wa takwimu zitakazosaidia
kufanikisha utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
“Leo
tumekutana hapa kwa pamoja ili kujadili namna bora ya upatikanaji wa
takwimu kwa ajili ya kupima na kutathmini utekelezaji wa viashiria vya
Malengo ya Maendeleo Endelevu na Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa
katika sekta ya Ukuaji Uchumi, Ajira na Ushindani wa Kiuchumi,” amesema
Mhandisi Mgalula.
Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Mipango, Wizara ya Fedha na Mipango Mhandisi Happiness Mgalula akizungumza wakati akifungua warsha ya siku mbili ya wadau wa takwimu waliokutana kuanzia leo jijini Dr es Salaam katika ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere.
Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Irenius Ruyobya akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari wakati wa hafla ya ufunguzi wa warsha ya siku mbili ya wadau wa takwimu waliokutana leo jijini Dr es Salaam katika ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere.
Baadhi ya wadau wa takwimu waliokutana leo jijini Dar es Salaam katika warsha ya siku mbili ili kujadili namna bora ya upatikanaji wa takwimu kwa ajili ya kupima na kutathmini utekelezaji wa viashiria vya Malengo ya Maendeleo Endelevu na Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...