Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amepongeza hatua ambayo kampuni ya kutengeneza mabodi ya magari ya Dar Coach Ltd imefika y'all kutengeneza na kukarabati mabasi 11ya vyombo vya ulinzi na usalama.

Kati ya magari hayo magari matano yatakabidhiwa mwishoni mwa mwezi huu na mengine sita yatakabidhiwa. 

Makonda amesema mmiliki wa kampuni hiyo amethibitisha uzalendo wake na mchango wake katika kusaidia Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam  inayotaka kuona vyombo vya ulinzi na usalama wanakuwa na usafiri wa kisasa na uhakika ili kutekeleza majukumu yao. 
Jumla ya Sh milioni 830 mmiliki wa kampuni hiyo anatumia katika kukarabati magari yote 11ambapo baadhi yamenfenezewa mabodi mapya kwani yalikuwa yameharibika sana. 

Akizungumza leo baada ya kukagua magari hayo katika kampuni hiyo iliyopo Mwandege wilayani Mkuranga mkoani Pwani,Makonda amesema hatua ya ukarabati magari hayo umefikia pazuri na ameahidiwa kukabidhiwa baadhi ya magari hayo mwishoni mwa mwezi huu.

Amesema wakati matengenezo ya magari hayo unaendelea wapo watu kwenye mitandao ya kijamii wanalalamika kwanini yasinunuliwe magari mapya kwa madai gharama kubwa. "Wanaosema gharama ya kutengeneza magari ya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ni kubwa wafahamu tu gharama za kutengeneza magari haya amejitolea mmiliki wa Kampuni ya Dar Coach Ltd,

"Ameamua kutoa mchango wake kupitia utalaam alionao wa kutengeneza mabodi ya magari ya majeshi yetu ambayo tumemletea. Ni mlipa kodi mzuri na kazi anayofanya ipo katika ubora unaokubalika,"Hao wanaolalamikia ukubwa wa gharama pengine  hawalipi hata kodi zaidi ya maneno tu.  Huyu ametusaidia na tunathamin mchango wake kwetu,"amesema. 
 Baadhi ya magari ya vyombo vya ulinzi na usalama ambayo yanaendelea kutengenezwa ambayo yalipelekwa yakiwa yameharibika kabisa 
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akizungumza leo wilayani Mkuranga mkoani Pwani wakati alipoenda kukagua magari 11 ya vyombo vya ulinzi na usalama yanayotengenezwa na Kampuni ya  Dar Coach. 
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akipewa maelezo leo na Mkurugenzi wa kampuni ya Dar Coach Manmeet Lal kuhusu hatua waliyofikia katika kufanya matengenezo ya magari 11 ya vyombo vya ulinzi na usalama
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akikagua magari 11 ya vyombo vya ulinzi na usalama ambayo yanatengenezwa mabodi yake yaliyokuwa yameharibika.Matengenezo hayo yanafanywa na Kampuni ya Dar Coach Ltd
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akikagua moja ya gari la Jeshi la Magereza leo inayofanyiwa matengenezo na Kampuni ya Dar Coach Ltd.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...