Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Ikiwa ni katika kuhakikisha anabeba kiatu cha ufungaji bora msimu wa 2017/18 mshambuliaji wa Simba , Emmanuel Okwi leo ameweza kuifungia timu yake magoli 2 na kujiweka juu ya msimamo.

Okwi aliyefikisha magoli 10 ikiwa ni muda mrefu toka awe na ukame wa magoli huku na kuamsha mbio za ufungaji bora.

Katika mechi dhidi ya Singida, Okwi aliyeingua katika dakika ya 65 akichukua nafasi ya Mzamiru Yassin aliweza kuandika goli la 3 kwa timu yake kwenye dakika ya 75 akipokea pasi ya Kichuya.

Dakika ya 81, Okwi anaandika goli la 4 na la 10 kwa upande wake akipokea pasi ya Said Ndemla na kuzidi kudidimiza matumaini ya Singida United.

Awali Okwi alikwama akiwa na mabao nane kwa kipindi kirefu hadi mshambuliaji wa Mbao FC, Habibu Kiyombo akafikisha mabao 7.

Simba imeweza kuimaliza Singida United kwa mabao 4-0 katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam goli la kwanza likifungwa dakika ya 3 na Shiza Kichuya na la pili dakika ya 25 na Asante Kwasi na kuendelea kusalia kileleni kwa alama 29 akifuatiwa na Azam yenye alama 27.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...