NA TIGANYA VINCENT,RS-TABORA

KANISA la Tanzania Assemblies of God (TAG) linatarajia kufunga na kuomba kwa muda wa siku 21 nchini kote kwa ajili ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na mihili mitatu ya Serikali kuanzia Jumatatu ijayo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Tanzanaia Askofu Dkt Barnabas Mtokambali wakati wa uzinduzi wa Chuo cha Biblia (Western Bible College) kilichojengwa Wilayani Uyui na Uzinduzi wa Shule ya Seminari ya Ushindi inayojengwa katika Manispaa ya Tabora.

Alisema kuwa kuanzia Jumatatu (22 January 2018) kitakuwa ni kipindi cha kuanza kufunga na maombi ya katika Makanisa ya TAG nchi nzima waumini wake watafunga na kuomba katika maombi yatakayojulikana kama maombi ya Daniel.

Askofu Mkuu wa TAG Askofu Dkt .Mtokambali alisema kuwa katika maombi hayo mojawapo ya ajenda ni kumwombea Rais Magufuli na Mihimili yote ya serikali ikiwa ni Serikali, Mahakama na Bunge ili aendelee kuwatumikia Watanzania vizuri kama alivyoanza.

“Mkuu wa Mkoa umeleta ombi lako wakati muafaka la kutaka Kanisa limuombee Rais katika kazi nzuri anazowafanyia Watanzania…Majenerali wa Bwana Yesu wa Kanisa letu wapo hapa kuanzia Jumatau ya tarehe 22 Januari 2018, Makanisa yetu yote tutakusanyika makanisani kwa ajili ya kufunga na kuomba” alisema Askofu Mkuu huyo wa TAG.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...