TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevikumbusha vyama vya siasa ambavyo vimesimamisha wagombea ubunge na udiwani katika majimbo mawili na kata tisa kuwa kesho (Februari 10) ndio siku ya mwisho ya kuwasilisha orodha ya mawakala wao kwa wasimamizi wa uchaguzi.

Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Bw. Ramadhan Kailima amesema hatua hiyo ni kwa mujibu wa kifungu namba 57 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi (Sura ya 343) na kifungu namba 58 cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa (Sura ya 292) ambazo zinabainisha kuwa majina ya mawakala  wa vyama vya siasa yanatakiwa kuwasilishwa kwa msimamizi wa uchaguzi siku saba kabla ya uchaguzi.

“Uchaguzi utafanyika tarehe 17 Februari 2018, hivyo siku saba kabla ya uchaguzi ni kesho (tarehe 10 Februari), hivyo nivisihi vyama vyote vya siasa vilivyosimamisha wagombea, kama vikitaka kuweka mawakala  kwenye uchaguzi huo, vipeleke orodha yao yaani utambulisho wa barua na kesho Jumamosi ndio siku ya mwisho.

“Ikifika tarehe 11 yaani Jumapili wasimamizi wa uchaguzi hawataruhusiwa kupokea orodha ya mawakala wa vyama vya siasa,” amesisitiza Kailima na kuongeza kuwa orodha hiyo ya mawakala kwa mujibu wa sheria iwe inaonesha jina la wakala, anuani yake na kituo ambacho chama kimependekeza wakala aende kusimamia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...