Na Ripota Wetu,Globu ya jamii.
WAZIRI wa Mambo ya ndani, Dk.Mwigulu Nchemba amewataka wanafunzi kuachana na harakati za kutengeneza taswira mbaya za Serikali badala yake kuwa na mitazamo chanya.
Dk.Mwigulu ameyasema hayo jana katika kongamano la UNILIFE lililofanyika Chuo cha Biashara (CBE), ambalo liliandaliwa na Mbunge wa Viti maalum, Ester Mmasi.
Amesema wanafunzi hawatakiwi kufanya harakati ili wawe adui wa Serikali kwani yenyewe haina muda wa kushughulikia mashinikizo ya wanafunzi.
"Nilishawahi kufanya harakati nikiwa chuoni na nilipewa jina la Chifu..majina yangu yamekuja kujulikana nikiwa serikalini lakini nilikuwa napinga baadhi ya ajenda za Taifa ambazo niliona hazina manufaa," amesema Dk. Mwigulu.
Amesisitiza wanafunzi wengi kwa sasa wamekuwa wakiitafuta taswira mbaya ya Serikali bila kuangalia masuala mengine yanayopaswa kuungwa mkono.
"Kuwa kijana mwema chuoni sio kwa kuwa kimya bali kuwa na mitazamo chanya na ukiona mwanazuoni anabisha jambo jema ujue kuna kasoro," amesema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...