Benki
ya Eco nchini Tanzania kuanzia mwaka huu inaanzisha mpango wa kutoa
zawadi ya ufadhili kwa wasichana wanaofanya vyema katika masomo yao
kwenye shule za serikali.
Aidha
pamoja na ufadhili huo ili kuwaweka katika hali ya kuwa na uzoefu na
kazi zao wanazosomea, watakuwa wanahakikisha wakati wa likizo
wanawafanyia mpango wa kujishughulisha na kazi hizo ili kuwa na uzoefu.
Hayo
yamesema na Mkurugenzi Mkuu benki hiyo nchini Mwanahiba Mzee wakati wa
hafla ya mchapalo iliyofanyika hoteli ya Serena kusherehekea mafanikio
ya mwanamke katika Siku ya Wanawake duniani mwishoni mwa wiki.
Alisema
taasisi yake inaona umuhimu wa kumwezesha mtoto wa kike kusonga mbele
kama moto wa taasisi hiyo ya kifedha unavyosema ‘press for progress’
ikimaananisha kujikita katika kutafuta maendeleo.
Alisema
mwanamke anafanyakazi nyingi hivyo ni vyema kumwandaa tangu mapema ili
kujua majukumu yake kama mzalishaji mkuu kwenye familia.
Alisema
kwa sasa hawajaamua wanaanzia ngazi gani za ufadhili, lakini wanataka
kufanya kitu tofauti chenye kulenga kupromoti maendeleo ya mtoto wa kike
kama maazimio ya Beijing yanavyotaka kufikia asilimia hamsini kwa
hamsini katika ngazi za kiutendaji.
Mkurugenzi Mkuu Ecobank Tanzania, Mwanahiba Mzee akizungumza kabla ya mgeni rasmi ambapo alielezea kwa undani safari ya maisha kama mwanamke wakati hafla mchapalo ya kusherehekea mafanikio ya mwanamke katika Siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Eco Bank Tanzania na kufanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mgeni rasmi Mwanasiasa Mkongwe nchini na mpigania haki za wanawake, Mama Getrude Mongella akitoa nasaha zake kwa wageni waalikwa na wafanyakazi wa Eco Bank Tanzania (hawapo pichani) wakati wa hafla mchapalo ya kusherehekea mafanikio ya mwanamke katika Siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Eco Bank Tanzania na kufanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkuu
wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Vodacom Tanzania, Nandi Mwiyombela
akijitambulisha na ku-‘share’ uzoefu sambamba na kubadilishana mawazo
wakati wa hafla mchapalo ya kusherehekea mafanikio ya mwanamke katika
Siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Eco Bank Tanzania na kufanyika
katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...