KIKOSI Cha Mabingwa wa soka nchini na ambao wapo kileleni mwa msimamo wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara, Yanga SC , kimeondoka leo saa 10:15 alfajiri kikielekea Nchini Botswana kuwafuata Township Rollers ukiwa ni mchezo wa marudiano wa michuano ya klabu bingwa barani Afrika.
Wachezaji 20 na viongozi 11 pamoja na wengine 8 ambao ni benchi la ufundi ambao wapo katika kikosi kamili cha msafara huo.
Ambapo katika mchezo uliopita uliokuwa wa aina yake kati ya timu hizo mbili ambao mtanange huo uliomalizika kwa dakika 90 na Yanga alichezeshwa Makhirikhiri na kulazwa chali kwa mabao 2-1 katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Katika Mchezo huo wa marudiano wakilishi kutoka Tanzania Yanga anakabiliwa na kibarua kizito kwa kutakiwa kupata ushindi mnene ili kusonga mbele na michuano hiyo.
Mtanange huo wa marudiano wa vuta nikuvute kati ya Mabingwa wa Tanzania bara Yanga dhidiTownship Rollers utarindima huko Nchini Botswana tarehe 17 machi mwaka huu ikiwa kila timu ikihitaji ushindi mnono ili kusonga mbele zaidi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...