Na Daudi Manongi,MAELEZO.

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi ) mhandisi Joseph Nyamhanga amewataka wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara hiyo na watumishi wote kutimiza wajibu wao kwa kutumia muda wa kazi ipasavyo kwa kufanya kazi kwa bidii.

Ameyasema hayo leo wakati akizindua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Sekta ya Uchukuzi leo Mkoani Dodoma.

Aidha mhandisi Nyamhanga amesema kuwa Wizara (Sekta ya Uchukuzi) inatambua mchango mkubwa wa wafanyakazi wa ngazi zote katika kufikiwa kwa maamuzi mbalimbali ya kisera na kitaalam na hivyo kufanikisha shughuli za sekta hiyo hali inayochochea Sekta ya Uchukuzi na utabiri wa hali ya hewa kutoa Huduma zenya ubora wa hali ya juu ndani na nje ya nchi.

Akifafanua mhandisi Nyamhanga amesema kuwa sekta ya Uchukuzi na Tabiri za Hali ya hewa zinatakiwa kutoa huduma zenye ubora wa kiwango cha juu ndani na nje ya nchi.

“Dhana hii ya ushirikishwaji wa wafanyakazi ni muhimu sana kwa jumuiya yeyote na katika ngazi yeyote,hivyo
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng.Joseph Nyamhanga (Kulia) akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano(Sekta ya Uchukuzi) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara hiyo Dkt.Leonard Chamuriho mkataba wa Baraza la Wafanyakazi mara baada ya kufungua na kuzindua mkutano wa Baraza hilo leo Mkoani Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng.Joseph Nyamhanga na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano(Sekta ya Uchukuzi) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara hiyo Dkt.Leonard Chamuriho na Viongozi wengine wa Baraza hilo wakiimba wimbo wa Solidarity Forever wakati wa Ufunguzi na Uzinduzi wa Baraza hilo leo Mjini Dodoma. Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng.Joseph Nyamhanga na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo leo Mkoani Dodoma. Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano(Sekta ya Uchukuzi) wakisIkiliza hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng.Joseph Nyamhanga (hayupo pichani) wakati akizindua na kufungua mkutano wa Baraza hilo Mkoani Dodoma. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...