Na Veronica Simba – Kigoma
Wachimbaji wa Madini wadogo wa Mkoa wa Kigoma, wamemweleza Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo changamoto mbalimbali zinazowakabili katika shughuli zao na kumwomba awasaidie kuzitatua.
Walimweleza changamoto hizo katika kikao maalum, Machi 3 mwaka huu, wakati Naibu Waziri alipowatembelea akiwa katika ziara ya kazi mkoani humo.
Miongoni mwa changamoto kubwa waliyoitaja ni kuhusu vibali vya kusafirisha madini ghafi nje ya nchi; ambapo Naibu Waziri aliwataka kuwa wavumilivu kwani Serikali inakamilisha mchakato wa kuandaa Mwongozo maalum utakaopambanua kila aina ya madini yaliyo nchini na yanapaswa kusafirishwa yakiwa katika hali gani. 
“Unajua, Madini yanatofautiana, na uchakataji wake unatofautiana. Hivyo tumeona tuandae Mwongozo utakaoondoa mkanganyiko huo na kuwarahisishia kujua Madini gani yanapaswa kuongezewa thamani kwa kiwango kipi ili uruhusiwe kuyasafirisha nje ya nchi.”
Alisema kuwa, Mwongozo huo utatolewa hivi karibuni na hivyo Serikali itaanza tena kutoa vibali vya usafirishaji Madini nje ya nchi.
Vilevile, wachimbaji hao walitaja changamoto nyingine kuwa ni upatikanaji wa Ruzuku ambapo pamoja na kulalamikia Serikali kusimamisha zoezi hilo, lakini pia walidai kuwa wakati ikitolewa, wahusika hawakutenda haki.
“Wasiokuwa na vigezo ndiyo walikuwa wakipatiwa Ruzuku ilhali wenye vigezo wakinyimwa,” walilalamika.
Akizungumzia suala hilo, Naibu Waziri aliwaeleza kuwa Serikali iliamua kusimamisha kwa muda zoezi la utoaji Ruzuku kutokana na kugundua udhaifu katika zoezi husika ikiwemo baadhi ya wanufaika kutumia Ruzuku waliyopewa kwa mambo yao binafsi tofauti na masharti yake. Hata hivyo, alisema kuwa Ruzuku itaanza kutolewa tena baada ya Serikali kujiridhisha kuwa itatumika vema.
Kuhusu suala la wenye vigezo kunyimwa Ruzuku na wasio na vigezo kupatiwa; Naibu Waziri alisema Serikali itafuatilia na kuchunguza kwa ukaribu ili kuwabaini watumishi wa umma na wengine wanaoshirikiana nao katika kupindisha utaratibu uliowekwa kwa sababu wanaozijua wao. 
“Tukiwabaini tutawachukulia hatua kali za kisheria. Nanyi tunawaomba mtuletee aina yoyote ya ushahidi unaoweza kutusaidia kuthibitisha madai yenu ili kwa pamoja tukomeshe tatizo hilo.”
 Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akizungumza na wachimbaji madini wadogo wa Mkoa wa Kigoma, wakati wa ziara yake ya kazi mkoani humo, Machi 3 Mwaka huu.
 Katibu wa Kikundi cha Wachimbaji Wadogo wa Madini Mkoa wa Kigoma, Iddi Lugundana, akisoma Risala ya Kikundi hicho mbele ya Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo (hayupo pichani), wakati alipowatembelea na kuzungumza nao, akiwa katika ziara ya kazi mkoani Kigoma, Machi 3 Mwaka huu.
Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo na Ujumbe wake, wakikagua Kiwanda cha Kuchakata Chokaa kinachomilikiwa na Kikundi cha Wachimbaji Wadogo wa Madini Mkoa wa Kigoma, kilichopo Eneo la Simbo, Machi 3 Mwaka huu.

KUSOMA ZAIDI  BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...