Aliyekuwa Mkurugenzi wa Tantrade Tanzania,Jacqueline Maleko akizungumza wakati wa usiku wa Wanawake na tunzo kwa Mwanamke aliyefanikiwa kwa mwaka 2018 iliyoandaliwa na Taasisi ya Shangwe ambapo wanawake kutoka sehemu mbalimbali walikutana na kuzungumza mambo ya ujasilimali na namna ya kuvuka kutoka hatua moja hadi nyingine.
Mkurugenzi wa Taasisi ya I-learn East Afrika ,Noela Bomani(Kulia) akikabidhi tuzo kwa Mwanamke aliyefanya vizuri na kuwa kivutio katika mafanikio yake katika kipindi cha mwaka 2017/2018 Joyce Ibengwe ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko Kutoka kwa Taasisi ya waajiri nchini(ATE).
Mshindi wa Tuzo ya Mwanamke aliyefanikiwa kwa mwaka 2017/2018 Joyce Ibengwe ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko Kutoka Tasisi ya waajiri nchini(ATE),akizungumza namna alivyopitia mpaka kufikia hatua hiyo kutoka kuitwa mama na watu mpaka mke wa mtu.
Meneja Bima ya magari kutoka shirika la Bima ya Taifa (NIC) Emakulata Mwaitege, akizungumza umuhimu wa Wanawake kujiwekea bima katika biashara zao na maisha yao ili waweze kusimama tena pindi majanga yanapowakuta.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...