MBUNGE wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam Maulid Mtulia (CCM), ametembelea maeneo ambayo yamekumbwa na mafuriko ya maji huku akitumia nafasi hiyo kutoa pole kwa wananchi wa jimbo hilo ambao wameathirika kwa namna moja au nyingine na mvua za masika huku akiishauri Halmashauri Manispaa ya Kinondoni kutafuta suluhu ya kudumu ili wananchi wabaki salama.

Pia amesema mbali ya kutoa pole atatumia fedha za Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kukodisha mashine za kunyonya maji pamoja na fedha ya kununua mafuta ili maji ambayo bado yapo kwenye makazi ya wananchi wake yaondolewe huku akitoa katazo la watu wasiendelee kujenga kwenye bwawa la Tengeza wala kutupa taka kwani athari zake ni kubwa kwa wananchi walio wengi.

Mbunge Mtulia amesema hayo jana jimboni kwake Kinondoni baada ya kufanya ziara ya kukagua maeneo ambayo yamekumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua za masika katika eneo la Kata ya Msisiri A,Msisiri B na Kambangwa ambapo pia ameshuhudia baadhi ya watu kujenga makazi kwenye bwawa la Tengeneza na matokeo yake maji kukosa pakwenda na hivyo kuharibu makazi ya watu.

Pia ametembelea baadhi ya nyumba za wananchi wa maeneo hayo ambapo zaidi ya asilimia 70 ya makazi ya watu yamekumbwa na mafuriko ambapo akatumia nafasi hiyo kuiomba Halmashauri ya Kinondoni kurekebisha mitaro iliyopo ili maji yapite kwa urahisi huku akitoa ombi la kuchimbwa kwa mitaro mikubwa ambayo itakuwa suluhu ya maji kutokwenda kwenye makazi ya watu kama ilivyo sasa.
ms1
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa , mtaa wa Msisiri A Jumanne Mbena akielezea changamoto za mafuriko ambazo zimesababishwa na baadhi ya wananchi kujenga kwenye Bwawa Tengeneza lililopo eneo la Msisiri A kwa Mbunge wa jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia(CCM),akifanya ziara ya kukagua maeneo ambayo yamekumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua za masika katika en eo la Kata ya Msisiri A,Msisiri B na Kambangwa
ms2
Mbunge wa jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia(CCM),akizungumza wakati alipofanya ziara ya kukagua maeneo am bayo yamekumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua za masika katika en eo la Kata ya Msisiri A,Msisiri B na Kambangwa
ms5
Muonekano wa maji yaliyozingira nyumba za wakazi wa Kata za Msisiri A na B na Kambangwa katika jimbo la Kinondoni jijini Dar es salaam.
ms6
Mbunge wa jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia(CCM),akipita kwa tabu wakati  alipofanya ziara ya kukagua mae neo ambayo yamekumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua za masika katika en eo la Kata ya Msisiri A,Msisiri B na Kambangwa
ms8
Mbunge wa jimbo la Kinondoni Maulid Mtulia(CCM),akiangalia moja ya madimbwi yaliyojaa maji mtaani alipo fanya ziara ya kukagua maeneo ambayo yamekumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua za masika katika eneo la Kata ya Msisiri A,Msisiri B na Kambangwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...