Assalaam Aleikum.

Salaam zangu za Mei Mosi

Kwanza sote tumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma anaendelea kutupa uhai na uzima hadi siku ya leo.
Hakika pumzi hii ndio inatufanya tufurahi na kuhuzunika pamoja,pia ndio inayotufanya tuweze kuandika na kusoma maandiko mbalimbali ikiwemo andishi hili dogo

Jana pale uwanja wa taifa palifanyika mechi kubwa kabisa ktk ukanda huu wa Afrika Mashariki. Simba na Yanga zote za hapa jijini Dar.

Sio vyema kurejea kuwapa matokeo ila Alhamdulillah klabu yangu ya Simba imefanikiwa kushinda na kujisogeza karibu kabisa na ubingwa wa ligi kuu nchini

Nimeandika kujisogeza kwa kuwa bado hatujatwaa ubingwa.kwa sasa tunahitaji points tano tu ili tuweze kutawazwa ubingwa huu unaosubiriwa kwa hama na washabiki wote kote nchini

Kiukweli hzi points tunazohitaji tutazisaka kwa tahadhari zote na kwa kutambua kiu ya wanasimba.. tutaingia kwenye michezo ilobaki kwa nguvu kubwa na kwa umakini wa hali ya juu,sambamba na kuwaheshimu wapinzani wetu

Ukiachana na hayo nna vitu vwili very special nataka kuvisema hapa

Kwanza ni shukran kwa washabiki wetu..ktk maisha yangu yote nilioishi sijapata kuona washabiki kama wa Simba..
Ni watu wasikivu mno na wenye subira na upendo wa hali ya juu,ni watu wanaopenda futboll halaf ndio timu yao,wana ustaarabu uliopitiliza na wenye mapenzi yasio na shaka kwa klabu yao,

Kwenye ustaarabu huwa natolea mfano wa kitendo cha kutoa back pass kwa mchezaji Hassan kesi wakati akiichezea Simba kwa Donald Ngoma wa Yanga na kutufunga goli la kizembe zaid ktk historia ya derby hii

Inawezeka kabisa ilikuwa ni bahati mbaya,ila kilichostaajibisha muda mchache ujao mchezaji huyo alihamia Yanga tena kwa maneno mabaya ya dharau na kebehi..naapa Wallah kitendo kile ingekuwa kwa wenzetu kessi angeuhama mji huu na kurudi Morogoro (tamka Mrogoro)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...