Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Tanzania VETA wameshiriki kongamano la elimu kupitia mtandao yenye lengo la kuhamasisha ubunifu kwa vijana na kuonesha jinsi kijana anavyoweza kusoma kwa kujitengemea kwa kutumia ubunifu wa  aplikesheni ya VSOMO inayotoa  elimu kwa mtandao.

Kwa miaka miwili sasa, VETA kupitia applikesheni ya VSOMO imekuwa ikitoa elimu kupitia mtandao kwa wanafunzi ambao wanataka kupata elimu ya ufundi stadi kwa udhamini wa Airtel Tanzania.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa kongamani hilo, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema kampuni ya Airtel iliamua kuwa mmoja wa wadau wa teknolojia hii ya kutoa elimu ya VSOMO ikiwa ni moja wa mkakati wake wa kurudisha sehemu ya faida yake katika kusaidia Jamii. Kwa kuweza kutambua umuhimu wa Jamii inayotuzunguka, tuna miradi ya kusaidia vijana kujikwamua yenye lengo ya kuwapa vijana ujuzi ili wajiajiri au wapate ajira kwenye sekta mbali mbali ili kuunga mkono juhudi za serikali za kujenga uchumi wa viwanda.

Airtel Tanzania inayo furaha kuona kuwa matumizi ya smartphone yakiwa ni darasa au ikiwa ni moja ya njia ya kutumika kupata elimu ya ufundi. Hii haiukuwa rahisi kufanya peke yetu ndio sababu tuliamua kushirikiana na VETA kama taasisi ya serikali yenye mamlaka ya kutumia elimu ya ufundi hapa nchini huku DTBi wakiwa ndio waliombuni applikesheni ya VSOMO, alisema Singano.

Airtel na washirika wake VETA na DTBi kwa sasa wana utaratibu mpya wa malipo kwa awamu ili kuwezesha wanafunzi wanaotaka kupata elimu ya ufundi stadi kufanya bila kupata changamoto za kulipa karo, aliongeza Singano.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano akitoa mada wakati kongamano la elimu kupitia mtandao yenye lengo la kuhamasisha kusoma kwa kujitengemea kwa miongoni mwa vijana hapa nchini kupitia teknologia ya VSOMO. Kongamano hilo liliandaliwa na Airtel Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Tanzania VETA na DTBi.
 Godfrey Magila kutoka taasisi ya DTBi akitoa mada wakati kongamano la elimu kupitia mtandao yenye lengo la kuhamasisha kusoma kwa kujitengemea kwa miongoni mwa vijana hapa nchini kupitia teknologia ya VSOMO. Kongamano hilo liliandaliwa na Airtel Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Tanzania VETA na DTBi
 Mratibu wa VSOMO kutoka Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Tanzania VETA Charles Mapuli  akitoa mada wakati kongamano la elimu kupitia mtandao yenye lengo la kuhamasisha kusoma kwa kujitengemea kwa miongoni mwa vijana hapa nchini kupitia teknologia ya VSOMO. Kongamano hilo liliandaliwa na Airtel Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi Tanzania VETA na DTBi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...