Na Munir Shemwea, Tabora
Kamishna
Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi Idrisa Keyera amesema manispaa ya
Tabora pekee inadai zaidi ya shilingi bilioni sita kwa wamiliki wa ardhi
na mashamba mkoani humo kama kodi ya ardhi.
Kayera
alisema hayo jana wakati akizungumza na watendaji kata wa Manispaa ya
Tabora alipokutana na watendaji hao kuhamasisha ulipaji wa kodi ya ardhi
na mashamba katika mkoa huo, mkutano uliofanyika ukumbi wa VETA Tabora.
Alisema,
mpaka kufikia sasa katika manispaa ya Tabora zimekusanywa jumla ya
shilingi bilioni 3.2 ikiwa ni pungufu ya malengo waliyojiwekea ya
kukusanya shilingi bilioni nne katika mwaka huu wa fedha unaoishia juni
mwaka 2018.
Alisema,
kanda yake inayohusisha mikoa ya Tabora, Shinyanga, Kigoma na Katavi
imeanza kuchukua hatua kwa wadaiwa sugu wa kodi za ardhi kwa kuwapatia
hati za madai ambapo wahusika watatakiwa kulipa madeni yao ndani ya wiki
mbili na wasipofanya hivyo wanapelekwa mahakamani na huko vifaa vyao au
nyumba zitauzwa kufidia deni huku umiliki nyumba ama shamba ukifutwa.
‘’Unapopelekwa
mahakamani uwezekano wa kushinda haupo na pia itakulazimu kulipa
gharama za madadlali kwa kushindwa kulipa’’ alisema Kamishana Msaidizi
Kayera.
Kwa
mujibu wa Kayera, kikao chake na watendaji wa kata za manispaa ya
Tabora ni moja ya harakati za ofisi yake ya Kanda ya magharibi
kuhakikisha kodi ya serikali inapatikana sambamba na kuwashirikisha
watendaji kuwatambua na kuwapelekea hati za madai wadaiwa sugu wa kodi
ya ardhi katika mitaa yao ili kuwabana waweze kulipa madeni yao.
Aidha,
Kamishna Msaidizi wa ardhi Kanda ya Magharibi alisema, utaratibu wa
kulipa kodi ya ardhi kwa sasa ni rahisi kwani unaweza kulipia kwa njia
ya simu na malipo hayo yanafanywa na wananchi waliopimiwa maeneo yao
ingawa serikali iko katika hatua za kuhakikisha maeneo yote ya mijini
hata yale yasiyopimwa wamiliki wake wanalipa kodi ya ardhi.
Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi Idrisa Kayera akizungumza na watendaji wa Kata za Manispaa ya Tabora jana wakati wa kampeni ya kuhamasisha ulipaji wa kodi ya ardhi katika kanda hiyo mkoani Tabora, kampeni inayoendeshwa na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kushoto ni Mwanasheria wa Kanda Ramadhani Jongo.
Watendaji wa Kata za Manispaa ya Tabora wakimsikiliza Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Kanda ya Magharibi Idrisa Kayera (hayupo pichani) wakati wa kampeni ya kuhamasisha ulipaji kodi ya ardhi katika kanda ya magharibi mkoani Tabora, kampeni inayoendeshwa na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mmoja wa watendaji wa kata za Manispaa ya Tabora akichangia maoni wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa kulipa kodi ya ardhi kanda ya magharibi ulioendeshwa na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...