Kampeni ya Juma ya Elimu Duniani huadhimishwa duniani kote kati ya mwezi wa nne na wa tano. Nchini Tanzania Maadhimisho haya huratibiwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TENMET) Ikishirikiana na wadau mbalimbali wa elimu, serikali na taasisi binafsi.

Kwa  Mwaka 2018 maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa yamefanyika Wilaya ya Mkalama, Mkoa wa Singida kuanzia tarehe Mei 14 hadi Mei 18 2018 ambapo Mgeni rasmi katika sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa alikua Mkuu wa Mkoa wa Singida Mh. Dk Rehema Nchimbi.

Akisoma majumuisho ya uhamasishaji wa juma la Elimu wilayani Mkalama Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania Dk. John Kallage alielezea mada ya Mwaka huu Kitaifa ni “Uwajibikaji wa pamoja kwa Elimu Bora kwa wote” na kwa wilaya ya Mkalama uhamasishaji ulifanyika katika Shule za Msingi sita na Shule za Sekondari tatu  ambapo ni katika vijiji sita ambavyo ni Mbigigi, Kikhonda, Ikolo, Mwangeza, Malaja na Nyahaa. 

Wadau wa elimu walifanikiwa kufanya mikutano ya kijamii ikijumuisha wazazi, wanajamii na viongozi wa serikali ya kijiji, dini na watu mashuhuri ili kubaini na kuzitafutia ufumbuzi changamoto za Elimu kwa pamoja.

Wadau wa Elimu katika Ziara ya uhamasishaji wa Juma la Elimu katika wilaya ya Mkalama walibaini Changamoto mbalimbali ikiwemo Bajeti finyu ya Serikali isiyokidhi mahitaji ya Sekta ya Elimu, Upungufu Mkubwa wa  walimu  na hasa waalimu wa masomo ya Sayansi na walimu wa Kike, Upungufu wa madawati, Upungufu wa vitabu vya kiada na ziada, Miundombinu isiyokidhi mahitaji mfano Vyumba vya madarasa, Vyoo, Maji na Nyumba za walimu pamoja na uhaba wa miundombinu rafiki kwa watu wenye mahitaji maalumu.
Mkuu wa Mkoa wa Singida. Dk Rehema Nchimbi  akizungumza na wadau wa elimu, walimu pamoja na wanafunzi wakati wa  kufunga maadhimisho ya Juma la Elimu kitaifa iliyofanyika katika wilaya ya Mkalama mkoani Singida.
Mwenyekiti Wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania Dk John Kallage akitoa risala ya majumuisho ya uhamasishaji ya Juma la Elimu Kitaifa yaliyofanyika katika wilayani Mkalama mkoani Singida.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mh Dk Rehema Nchimbi akigawa mipira ya Miguu kwa baadhi ya wakuu wa shule za Msingi na Sekondari katika wilaya ya Mkalama ambayo iliyotolewa na Mtandao wa Elimu Tanzania wakati wa kilele cha Maadhimisho ya juma la elimu Kitaifa.
Mkuu wa Mkoa wa Singida. Dk Rehema Nchimbi akiendesha harambee ya kuchangia maboresho ya Elimu wilayani Mkalama wakati wa kilele cha juma la elimu yaliyofanyika wilayani humo.
Baadhi ya wanafunzi wakimuonyesha mabango yenye ujumbe wa Kuhamasisha Uwajibikaji wa Pamoja kwa Elimu Bora  wakati wa kilele cha juma la maadhimisho ya Elimu yaliyofanyika Wilayani Mkalama.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...