JOSEPH MPANGALA-MTWARA.      

Mtu mmoja aliyejulikana kwa Jina la Ahamad Salum mkazi wa Kata ya Namiyonga Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara ameuawa na Mke wake Sofia Swaleh  Kwa Kuchomwa Kisu Kifuani kutokana na Majibizano ya Kupika Chakula Kingine.

Uchunguzi wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa kabla ya Mauaji hayo kulitokea Ugomvi baina ya Marehem na Mkewe ambapo Marehem alipikiwa Chakula na baada ya Kula Hakushiba hivyo akashinikiza Mke wake kumuandalia Chakula kingine Ndipo Ugomvi ukaibuka,na Ndipo Mke wa Marehemu Sofia Swalehe akachukua Kisu na Kumchoma eneo la Kifuani na kupelekea Ahamad Salum kufariki dunia kutokana na kupoteza Damu Nyingi.

Akiongea na Waandishi wa Habari Ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara DCP Lucas Mkondya amesema Watu wawili wanashikiliwa na Polisi Mmoja ni Jirani, Mussa Bakari ambaye aliingia ndani ya Nyumba baada ya kusikia Ugomvi ukiendelea na akashirikiana na Mke wa Marehem Sofia Swalehe kuua.

Aidha Kamanda Mkondya amewataka wananchi kutumia Viongozi wa Kiserikali na Kidini kuweza kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili katika Jamii.

'Nitoe rai kwa wananchii Magomvi hayana tija wajaribu kukaa na Kususuluhisha sio mnakaa na kugombana kwa kitu Kidogo mpaka mnapoteza Maisha kwa kitu Kidogo kama Chakula"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...