………………
Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imetoa mafunzo ya uandishi wa habari za kitakwimu kwa wanachama wa chama cha waandishi wa habari Dodoma ili kuwaongezea uwezo wa uandishi mzuri wa habari za kitakwimu.

Mafunzo hayo ya siku mbili kuanzia tarehe 26 hadi 27 Mei, mwaka huu  yanayofanyika katika ukumbi wa Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) Jijini Dodoma yamefunguliwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi.  Zamaradi Kawawa kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara hiyo.

Akifungua mafunzo hayo Zamaradi Kawawa amesema kutokana na Wizara zote pamoja na baadhi ya Taasisi kuhamia Dodoma, Dodoma imekuwa ndio kitovu cha shughuli za Serikali kwa maana hiyo imekuwa chanzo kikuu cha habari zinazohusu Serikaki nchini hivyo basi majukumu ya vyombo vya habari vilivyopo mkoani Dodoma yameongezeka na yatazidi kuongezeka kadiri shughuli za Kiserikali  zinavyoongezeka.

“Hapana shaka yeyote kuwa watumishi wote wa vyombo vya habari vilivyopo Dodoma wanahitaji mafunzo kama haya kwa ajili ya kuimarisha weledi wao katika kuripoti matukio mbalimbali yanayotokea mkoani humu,” amesema Zamaradi.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO Bi.  Zamaradi Kawawa akifungua mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji  la Dodoma leo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi.
2
Mkurugenzi  Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt.  Albina Chuwa akisisitiza kuhusu namna idadi ya watu inavyoongezeka au kupungua wakati  wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
3
Mtakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Omary Mdoka akiwasilisha mada kuhusu ongezeko la watu  wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
4
Mwanasheria wa Ofisi ya  Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Oscar Mangula akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya takwimu ya mwaka 2015 wakati  wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
5
Mtakwimu  kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi.  Mariam Kitembe akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu hali ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi hapa nchini kwa kuzingatia utafiti uliofanyika mwaka 2016/2017 wakati  wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
6
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu  (NBS) Bw. Said Ameir akitoa maelezo kuhusu mafunzo ya siku mbili ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la  Dodoma leo.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...