Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (katikati) na Mbunge wa Bunge la Ireland, Mhe. Catherine Conolly (kulia) walipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Wabunge wa Bunge la Ireland walioambatana na Maafisa waandamizi kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali Ireland walioongozwa na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (kushoto kwake) walipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Ireland ambao pia ni Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Ireland, walioongozwa na Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Paul Sherlock (kulia) baada ya mazungumzo nao yaliyofanyika leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Ireland wakutana na kuzungumza na Mtandao wa Wabunge wanawake wa Bunge la Tanzania (TWPG) leo katika Ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma.
Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za serikali (PAC) kutoka Bunge la Ireland katika tukio lililofanyika leo nje ya Ukumbi wa Pius Msekwa Jijini Dodoma. Lengo likiwa ni kujenga urafiki na kubadilishana uzoefu katika utendaji wao wa kazi.

(PICHA NA DEONISIUS SIMBA - OFISI YA BUNGE)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...