Awamu
ya pili na mashindano yanayohusisha timu bora za Afrika
Mashariki-SportPesa Super Cup yanatarajiwa kuanza Juni 3-10, 2018 nchini
Kenya kwenye uwanja wa Kimataifa wa Moi uliopo Kasarani.Timu
zitakazoshiriki katika michuano hiyo kutoka Tanzania ni timu
zinazodhaminiwa na SportPesa ambazo ni Simba, Yanga, Singida United
pamoja na JKU (Jeshi la Kujenga Uchumi kutoka Zanzibar), wakati kutoka
Nairobi timu zitakazoshiriki ni Gor Mahia, AFC Leopards na Kariobangi
Sharks na Kakamega Homeboys.
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za SportPesa zilizopo Masaki, Dar es Salaam ambapo pia walikuwepo wawakilishi na viongozi kutoka TFF pamoja na viongozi wa timu za Simba, Yanga na Singida United Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti Bwana Tarimba Abbas alisema “michuano hii kuleta chachu na kumpata bingwa kwa upande wa Africa Mashariki”
Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za SportPesa zilizopo Masaki, Dar es Salaam ambapo pia walikuwepo wawakilishi na viongozi kutoka TFF pamoja na viongozi wa timu za Simba, Yanga na Singida United Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti Bwana Tarimba Abbas alisema “michuano hii kuleta chachu na kumpata bingwa kwa upande wa Africa Mashariki”
Matayarisho
ya mwaka huu yamefanyika mapema na ukiangalia muda wa kupewa na taarifa
mpaka kuanza ni zaidi ya mwaka mmoja, hivyo basi hakuna sababu kwa timu
zetu za Tanania zisifanye vibaya zaidi ya mwaka jana kwani matayarisho
yamefanyoka mapema na kwa hali hiyo timu zikifanya vibaya tutakuwa na
sababu za kuwalaumu.Kutakuwa na jumla ya timu nane za Afrika Mashariki
na mshindi wa michuano hiyo atacheza na moja kati ya timu iliyoshiriki
ligi kuu uingereza, Everton.
Timu zitakazoingia robo fainali kwenye mashindano haya watapata kiasi cha dola za kimarekani 2,500, nafasi ya nne timu itapata kiasi cha dola 5000, wakati nafasi ya tatu na wa pili dola 7,500 na 10,000 kila mmoja.Timu itakayoshinda itazawadiwa kiasi cha dola 30,000 na kupata nafasi ya kuchuana na timu ya Everton katika uwanja wa Goodison Park.Napenda kuwatakia kila la kheri timu zetu tatu zinazokwenda kutuwakilisha jijini Nairobi, natumaini zitatutoa kimasomaso kwa kufanya vizuri zaidi ya mwaka jana, wataiwakilisha nchi yetu vilivyo kwa kucheza kwa uweledi na nidhamu” alimaliza Ndugu Tarimba
Timu zitakazoingia robo fainali kwenye mashindano haya watapata kiasi cha dola za kimarekani 2,500, nafasi ya nne timu itapata kiasi cha dola 5000, wakati nafasi ya tatu na wa pili dola 7,500 na 10,000 kila mmoja.Timu itakayoshinda itazawadiwa kiasi cha dola 30,000 na kupata nafasi ya kuchuana na timu ya Everton katika uwanja wa Goodison Park.Napenda kuwatakia kila la kheri timu zetu tatu zinazokwenda kutuwakilisha jijini Nairobi, natumaini zitatutoa kimasomaso kwa kufanya vizuri zaidi ya mwaka jana, wataiwakilisha nchi yetu vilivyo kwa kucheza kwa uweledi na nidhamu” alimaliza Ndugu Tarimba
Kwa
upande wa timu ya Simba Ndugu Said Tulliy alisema “Napenda kuchukua
nafasii hii kuwataarifu wanasimba kuwa tunakwenda kushiriki mashindano
kama timu shindani na si timu shiriki na tunajua mwaka jana tulipata
nafasi kama hii lakini tuliipoteza na tusingependa kitu kama hicho
kijirudie.
Tumeona faida yake kutokana na jinsi wenzetu waliopita ni jinsi gani walivyofaidikakupitia mashindano hayo.Kama timu tumejiandaa na tuko tayari kuhakikisha tunalinda heshima ya Simba Sports Club na heshima ya Tanzania, tunakwenda na kikosi kamili ili kuhakikisha tunachukua ubingwa ili tuweze kushindana na timu iliyopangwa.
Tumeona faida yake kutokana na jinsi wenzetu waliopita ni jinsi gani walivyofaidikakupitia mashindano hayo.Kama timu tumejiandaa na tuko tayari kuhakikisha tunalinda heshima ya Simba Sports Club na heshima ya Tanzania, tunakwenda na kikosi kamili ili kuhakikisha tunachukua ubingwa ili tuweze kushindana na timu iliyopangwa.
Tunathibitisha
kuwa tutashiriki mashindano haya kwa sababu ni mashindano muhimu, tuko
tayari kwa ajili ya mashindano na timu yetu nzima na tuko tayari ya
kushinda” alimaliza Ndugu Said Tulliy.
“Changamoto
ya mashindano iko pale pale lakini kwa mwaka huu nia yetu kuu ni
kuchukua ubingwa ili kuleta heshima kimataifa” Charles Boniface Mkwasa
Yanga.
“Kwanza
napenda kuwashukuru SportPesa kwa sababu wamefanya timu yetu kujulikana
kwenye kila kona ya nchi, moja kati ya wadhamini wetu wa nguvu ambao
tunajivunia sana kutoka kampuni hii. Jambo kubwa tutakaloenda kulifanya
kwenye michuano hii kimsingi kwa mwaka huu tumeweza kushirikishwa mapema
ili tuweze kujipanga sisi kama timu lakini kikubwa zaidi ikumbukwe kuwa
Singida United ni timu pekee iliyofanikiwa kufika nusu fainali kwa hapa
Tanzania na mwaka huu tunaamini tutachukua kombe
Kwa
watanzania na watu wa Africa mashariki tunaombawatuunge mkono timu
yetu. Ningependa kuwaomba SportPesa kuhakikisha kanuni na sheria za
mpira wa miguu zinafatwa ili michuano hii iweze kumalizika
vizuri”–Shabani Mande Singida United.
Tunapenda
kuwashukuru SportPesa kwa kututambua na kutupa nafasi ya kushiriki
katika michuano hii na napenda kuwaahidi hatutawaangusha ingawa hii
itakuw mara ya kwanza kushiriki.” Maalim Masoud, Katibu wa klabu, JKU.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...