Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (wa tatu kushoto), akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. Mil.100, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi (wa tatu kulia), kwa ajili ya kusaidia ukarabati wodi ya wagonjwa wa moyo, katika Taasisi hiyo, Muhimbili jijini Dar es Salaam.Wengine pichani kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Huduma Mbadala wa Benki ya CRDB, Philip Alfred, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo na Kaimu Mkuu wa kitengo cha Ubora wa Huduma za Afya ya Moyo, Dkt. Tulizo Shemu, Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa pamoja na Mkurugenzi wa Wateja wadogo na wa kati wa Benki ya CRDB, Jessica Nyachiro.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza jambo katika mkutano wake na uongozi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ulioambatana na kuchangia fedha kiasi cha sh. mil 100 kwa ajili ya ukarabati wa wodi ya wagonjwa wa moyo, katika Taasisi hiyo, Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akizungumza jambo wakati akitoa taarifa ya Taasisi yake kwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei aliyeambatana na ujumbe wake.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...