SHIRIKA la Brac limetoa vifaa vya kazi vyenye thamani ya sh Mil 69 kwa wasichana 924 kwa ajili ya kuanza shughuli za ujasirimali ili kuweza kujikwamua kiuchumi .

Vifaa hivyo ambavyo vimetolewa maalum kupitia mradi wake wa kuwajengea uwezo na kujiajiri wasichana ambao wameshindwa kuendelea masomo ya sekondari mkoani Tanga.Akikabidhi msaada huo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa alisema kuwa vifaa hivyo vitaweza kuwasaidia wasichana hao kuweza kujiendeleza kiuchumi kwa kujihakikishi kipato chao.

“Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ili kuweza kufikia uchumi wa viwanda lakini kupitia Brac tunaona walivyofanikiwa kuwawezesha wasichana hao ili waweze kujikwamua kiuchumi”alisema DC Mwilapwa.

Kwa upande wake Mkurungenzi Mkuu wa Brac Assan Golowa alisema kuwa tayari mradi huo umefanikiwa kuwafikia wasichana 240 toka ulipoanzishwa mwaka 2016 mkoani humo.Alisema kuwa mradai huo unatoa fursa ya pili kwa wasichana walioshindwa kuendelea na masomo waweze kujifunza ujuzi wa mikono na kuweza kujiajiri ili kuweza kuwa wazalishaji mali.

“Mradi huu upo katika mikoa 23 hapa nchini lakini kwa mkoa wa Tanga umeonyesha mafanikio zaidi kutokana na muitikio mkubwa wa wasicahna kujivutika kujiunga na mradi huo”alisema Golowa.
 Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa vyenye thamani ya ya sh Mil 69 kwa wasichana 924 kwa ajili ya kuanza shughuli za ujasirimali ili kuweza kujikwamua kiuchum ambavyo ni vyerahani na madraya ya saloon na vifaa vyengine kushoto ni Mkurungenzi Mkuu wa Brac Assan Golowa.
Mkurungenzi Mkuu wa Brac Assan Golowa akizungumza katika halfa hiyo
PRO wa shirika la BRAC SEcilia Bosco akizungumza katika halfa hiyo
sehemu ya vyarahani vilivyotolewa
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akimkabidhi vifaa vya saloni moja wa wasichana waliopatiwa mafunzo na shirika la BRAC
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akiangalia baadhi ya vifaa v ya shuleni kabla ya kuvikabidhi kwa wahusika .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...