Mhandisi wa Mifumo ya dot TZ kutoka Tanzania Network Information Centre (TZNIC), Bw. Raymond Linus akiongea na wataalamu wa ICT na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa kuwa na kikoa cha .tz (.tz domain name) katika mkutano wa ICT uliofanyika Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA). Dot TZ registry imekua ikidhamini mikutano hii ya ICT kuelimisha wananchi juu ya faida ya kutumia kikoa cha .tz katika mawasiliano ya Intaneti.
Mkuu wa Idara ya Informatics wa Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA) Bi. Pamela Chogo akiwakaribisha wataalamu na wanafunzi wa ICT kwenye mkutano wa ICT uliofanyika Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA) Dr. Samwel Werema akizungumza na wanafunzi wa ICT kwenye mkutano wa ICT uliofanyika Chuo cha Uhasibu Arusha (AIA).
Wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha walioshiriki mashindano ya ICT (Arusha ICT Innovative Challenge 2018 – Jiji Hackathon) wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...