Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo ameziagiza halmashauri ambazo zinaendelea na ujenzi wa mabweni na madarasa kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wa kudato cha tano Julai mwaka huu kuongeza kasi ya ujenzi huo ili ziweze kuwapokea wanafunzi watakaopangwa katika shule hizo. 

Waziri Jafo aliyasema hayo leo mkoani Morogoro alipokuwa akikagua ujenzi wa shule ya wasichana ya Sokoine Memorial inayojengwa wilayani Mvomero. 

Alipokuwa wilayani humo, Waziri Jafo amemsisitiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mvomero kuongeza idadi ya mafundi ili kazi hiyo ifanyike kwa kasi pindi fedha zilizoombwa za umaliziaji sh.millioni 900 kutoka wizara ya elimu zitakapotolewa. 

Katika ziara hiyo, Jafo aliongozana na Mkuu wa mkoa Morogoro Dk.Steven Kebwe ambapo miradi mbalimbali ya elimu na afya ilikaguliwa ikijumuisha Sekondari mpya ya wasichana ya Sokoine Memorial,  kituo cha afya Chazi, Hospitali Teule ya Bwagala , pamoja na sekondari ya Lusanga.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akikagua ujenzi unaoendelea katika Shule ya Sokoine Memorial wilayani Mvomero
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akisisitiza jambo kwa viongozi na watendaji wa mkoa wa Morogoro na wilaya ya Mvomero wakati wa ukaguzi wa sekondari ya sokoine memorial
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo  akiongea na wananchi katika kituo cha afya Chazi wilayani Mvomero
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo  akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa afya wa Hopitali Teule ya Bwagala iliyopo Turiani wilayani Mvomero
Ukaguzi wa nyumba za watumishi ukiendelea katika sekondari ya sokoine memorial

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...