Jaji wa Mahakama Kuu ya Uganda, Mhe. Paul Gadenya akitia saini kitabu cha wageni pindi alipowasili katika Mahakama ya Wilaya Kigamboni kujionea jengo hilo la kisasa lililojengwa kwa teknolojia ya ujenzi ya Moladi, mbali na kutembelea jengo hilo Jaji Gadenya ametembelea Ofisi za Kitengo cha Maboresho ya Mahakama ‘JDU’ kupata taarifa ya maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika ndani ya Mahakama kwa lengo la kuboresha huduma za utoaji haki nchini, aliyesimama kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kigamboni, Mhe. Sundi Fimbo.
 Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kigamboni, Mhe. Sundi Fimbo, akimpitisha Mhe. Jaji Gadenya kukagua sehemu mbalimbali za jengo hilo la kisasa, aliyepo nyuma ya Mhe. Gadenya ni Mkurugenzi Msaidizi Ufuatiliaji na Tathmini, Mahakama, Bw. Sebastian Lacha. 
 Mhe. Jaji Gadenya (kushoto) akijadili jambo na wenzake, kulia ni Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kigamboni, Mhe. Sundi Fimbo na katikati ni Mkurugenzi Msaidizi Ufuatiliaji na Tathmini, Mahakama, Bw. Sebastian Lacha.
Picha ya pamoja nje ya jengo jipya la kisasa la Mahakama ya Mwanzo na Mahakama ya Wilaya Kigamboni, Mhe. Gadenya ameisifu Mahakama kwa maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika na ambayo tayari ameshafanyika kwa ustawi wa Wananchi.
(Picha na Mary Gwera, Mahakama)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...