*Asema heshima ya nchi ni kujitegemea

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
RAIS Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa amesema hakuna Mtu wa kutumwagia fedha kwa ajili ya maendeleo yetu, bali yataletwa kwa watu kufanya kazi na heshima ya nchi ni kujitegemea .

Mkapa ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati anazindua kitabu cha Hali ya umasikini hasa katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara na Afrika kwa ujumla.

Kitabu hicho kimeandikwa na aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu Balozi Martin Lumbanga. Kitabu hicho kimepewa jina la Global Poverty(The Case for Sab-Sahara Afrika)

Kabla ya kuzindua Kitabu hicho Mkapa amesema "Huu utamaduni wa kusubiri kumwambiwa fedha sijui umetoka wapi.Haipo hata katika Chama tawala ya kumwagia pesa."

Akasisistiza kwa kuhoji tena kwa Dunia hii ya Trump? "Lazima tufanye kazi kwa maendeleo yetu badala ya kusubiri fedha kutoka nje,"amefafanua Mkapa.

Mkapa anasema inashangaza unaposikia wapo wanaosubiri kumwagiwa fedha tena utasikia "Neema yaja .Haipo, heshima ya nchi ni kujitambua na kujitegemea."
Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa akizundua kitabu cha Global Poverty (The Case For Sub- Sahara Africa) pamoja na Mtunzi wa kitabu hicho Balozi Martine Lumbanga (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya kuchapisha vitabu ya Mkuki na Nyota Bw. Walter Bgoya(kulia), uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa JNICC jijini Dar es salaam leo.
 Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa  akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Global Poverty (The Case For Sub- Sahara Africa) uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa JNICC jijini Dar es salaam leo.
 Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa akionyesha kitabu cha Global Poverty (The Case For Sub- Sahara Africa) mara baada ya kukizindua kushoto ni Mtunzi wa kitabu hicho Balozi Martine Lumbanga na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya kuchapisha vitabu ya Mkuki na Nyota Bw. Walter Bgoya, Uzinduzi huo umefanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa JNICC jijini Dar es salaam leo.
Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa akipokea zawadi ya kitabu cha Global Poverty (The Case For Sub- Sahara Africa) na Balozi Martine Lumbanga mara baada ya Uzinduzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa JNICC jijini Dar es salaam leo.
 Mtunzi wa kitabu hicho Balozi Martine Lumbanga (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya kuchapisha vitabu ya Mkuki na Nyota Bw. Walter Bgoya, katika uzinduzi uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa JNICC jijini Dar es salaam leo.
Balozi Martine Lumbanga(kulia) akisaini kitabu cha mmoja wa wageni waliofika kwenye uzinduzi huo baada ya kukinunua.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...